أيد
Maoni ya Mwanasiasa kuhusu Mabadiliko ya Demografia
تم النشر بتاريخ 12 آذار 2024
Bodi ya Usimamizi imeunga mkono uamuzi wa Meta wa kuacha klipu ya video ambapo mwanasiasa wa Ufaransa Éric Zemmour anajadili mabadiliko ya kidemografia barani Ulaya na Afrika.
Muhtasari
Bodi ya Usimamizi imeunga mkono uamuzi wa Meta wa kuacha klipu ya video ambapo mwanasiasa wa Ufaransa Éric Zemmour anajadili mabadiliko ya kidemografia barani Ulaya na Afrika. Maudhui hayo hayakiuki Viwango vya Jumuiya kuhusu Matamshi ya Chuki kwa kuwa hakuna shambulio la moja kwa moja dhidi ya watu kulingana na sifa iliyolindwa kama vile rangi, kabila au asili ya taifa. Wengi wa Wanabodi wamepata kuwa kuacha maudhui hayo kunaambatana na majukumu ya Meta ya haki za binadamu. Hata hivyo, Bodi inapendekeza kwamba Meta inapaswa kuweka wazi kwa umma jinsi inavyotofautisha majadiliano yanayohusiana na uhamiaji na yale ya matamshi ya chuki, ikiwa ni pamoja na njama za chuki, kulenga watu kulingana na hali zao za uhamiaji.
Kuhusu Kesi
Mnamo Julai 2023, klipu ya video ambapo mwanasiasa wa Ufaransa Éric Zemmour anajadili mabadiliko ya kidemografia barani Ulaya na Afrika ilichapishwa kwenye ukurasa wake rasmi wa Facebook na mtumiaji ambaye ni msimamizi wa ukurasa huo. Klipu hiyo ni sehemu ya mahojiano kwenye video ndefu zaidi na mwanasiasa huyo. Kwenye video hiyo, Zemmour anasema: “Tangu kuanza kwa karne ya 20, idadi ya watu barani Afrika imeongezeka sana.” Anaendelea kusema kwamba huku idadi ya watu barani Ulaya ikisalia katika sawa ya takriban watu milioni 400, Idadi ya watu barani Afrika imeongezeka hadi watu bilioni 1.5, “kwa hivyo mizani ya nguvu imebadilika.” Manukuu yaliyo kwa Kifaransa yanasema kuwa katika miaka ya 1900 “wakati kulikuwa na Wanaulaya wanne kwa kila Mwafrika mmoja, [Ulaya] ilikuwa mkoloni wa Afrika,” na sasa “kuna Waafrika wanne kwa kila Mwanaulaya mmoja na Afrika inaikoloni Ulaya.” Ukurasa wa Facebook wa Zemmour una takriban wafuasi 300,000 huku chapisho hili likitazamwa takriban mara 40,000 kufikia Januari 2024.
Zemmour amewahi kupatikana na hatia kadhaa za kisheria, na kufunguliwa mashtaka zaidi ya mara moja nchini Ufaransa kwa kuchochea chuki za ubaguzi na kutoa maoni ya matusi ya kibaguzi kuhusu Waislamu, Waafrika na watu Weusi. Aliwania kuwa rais mwaka 2022 lakini hakufaulu zaidi ya awamu ya kwanza. Suala moja kuu katika kampeni zake za uchaguzi ni Nadharia ya Ubadilishaji Mkubwa, ambayo inahoji kwamba watu weupe kutoka Ulaya wanabadilishwa kwa kukusudia kikabila na kitamaduni kupitia uhamiaji na ukuaji wa jamii za wachache. Wataalamu wa isimu wanabainisha kuwa nadharia hii na maneno yanayohusiana nayo “yanachochea ubaguzi, chuki na vurugu dhidi ya wahamiaji, jamii za watu wasio weupe kutoka Ulaya na kulenga Waislamu kwa njia mahususi.” Video kwenye chapisho hilo haihitaji nadharia hiyo kwa njia mahususi.
Watumiaji wawili waliripoti maudhui hayo kwa kukiuka sera ya Meta dhidi ya Matamshi ya Chuki lakini kwa kuwa ripoti hizo hazikupewa kipaumbele cha ukaguzi ndani ya kipindi cha saa 48, zote zilifungwa kiotomatiki. Ripoti hupewa kipaumbele na mifumo otomatiki ya Meta kulingana na kina cha ukiukaji unaobashiriwa, urijali wa maudhui (idadi ya mionekano) na uwezekano wa ukiukaji. Mmoja wa watumiaji kisha akakata rufaa kwa Meta, hatua iliyosababisha mojawapo ya wahakiki binadamu wa kampuni hiyo kuamua kuwa maudhui hayakukiuka kanuni za Meta. Mtumiaji kisha alikata rufaa kwa Bodi.
Matokeo Muhimu
Wanabodi wengi walihitimisha kuwa maudhui hayo hayakiuki Viwango vya Jumuiya ya Meta kuhusu Matamshi ya Chuki. Klipu hiyo ya video ina mfano wa usemi unaolindwa (wenye utata) wa maoni kuhusu uhamiaji na haina mwito wowote wa vurugu, wala hautumii lugha ya moja kwa moja ya kudunisha au ya chuki dhidi ya vikundi vilivyo hatarini. Ingawa Zemmour amefunguliwa mashtaka kwa kutumia lugha ya chuki hapo awali na kauli mbiu kwenye video hii ni sawa na Nadharia ya Ubadilishaji Mkubwa, kweli hizi hazitoi sababu ya kuondolewa kwa chapisho ambalo halikiuki viwango vya Meta.
Ili kuwepo ukiukaji, ni sharti chapisho hilo lingejumuisha “shambulio la moja kwa moja,” hususan kutoa mwito wa “ubaguzi au utengaji” wa kikundi chenye “sifa iliyolindwa”. Kwa kuwa maoni ya Zemmour hayana shambulio lolote la moja kwa moja, na hakuna mwito wa wazi wa kutenga kikundi chochote kutoka Ulaya wala taarifa yoyote kuhusu Waafrika inayoweza kuainishwa kama kasumba yenye madhara, ubaguzi au shambulio lolote la moja kwa moja, hayakiuki kanuni za Meta za Matamshi ya Chuki. Mtazamo wa sera pia unabainisha wazi kwamba Meta huruhusu “maoni kuhusu na usutaji wa sera za uhamiaji,” ingawa jambo ambalo halijashirikiwa kwa umma ni kwamba kampuni hiyo inaruhusu miito ya kutengwa wakati sera za uhamiaji zinajadiliwa.
Hata hivyo, Bodi ina wasiwasi kwamba Meta haizingatii Waafrika kama kikundi chenye sifa iliyolindwa, kutokana na ukweli kwamba asili ya taifa, rangi na dini zinalinda chini ya sera za Meta na sheria ya kimataifa ya haki za binadamu. Waafrika wametajwa kote kwenye maudhui hayo na, katika video hii, wanatumika kama wandani wa Waafrika wasio weupe.
Bodi pia inazingatia ufaafu wa sera dhidi ya Watu na Mashirika Hatari katika kesi hii. Hata hivyo, wengi walipata kuwa chapisho hili halikiuki sera hii kwa sababu hakuna vipengele vya kutosha vya kulikagua kama sehemu pana ya Mtandao wa Njama Inayosababisha Vurugu. Meta inafafanua mitandao hii kama watendaji wasio wa serikali wanaotumia taarifa moja ya lengo, kuendeleza nadharia zisizo na msingi zinazodai kuwa njama za siri za watendaji wenye uwezo mkubwa zinasababisha matatizo ya kijamii na kisiasa na ambao wanahusishwa na mtindo wa madhara ya nje ya mtandao.
Wanachama Wachache wa Bodi walipata kwamba mbinu ya Meta ya kushughulikia maudhui yanayoeneza nadharia za njama zenye madhara haioani na malengo ya sera ambayo imeweka ili kuzuia mazingira ya utengaji yanayoathiri wachache wanaolindwa, mtandaoni na nje ya mtandao. Chini ya sera hizi, maudhui yanayohusisha dhana fulani za njama hudhibitiwa ili kulinda vikundi vya wachache wanaolindwa. Ingawa Wanachama hawa wa Bodi wanaamini kuwa usutaji wa masuala kama vile uhamiaji unapaswa kuruhusiwa,ni kwa sababu majadiliano yaliyokitwa kwenye ushahidi kuhusu mada hii ni muhimu sana kwamba kuenea kwa nadharia kama hizo za njama, kama vile Nadharia ya Ubadilishaji Kubwa, inaweza kuwa na madhara. Si sehemu za maudhui lakini jumla ya athari ya maudhui kama hayo yanaposhirikiwa kwa kiwango kikubwa na kwa kasi ya juu ambayo husababisha changamoto kubwa kwa kampuni za mitandao ya jamii. Kwa hivyo, Meta inahitaji kuunda upya sera zake ili huduma zake zisitumike vibaya na watu wanaoeneza nadharia za njama na kusababisha madhara ya mtandaoni na ya nje ya mtandao.
Meta imefanya utafiti kuhusu mkondo wa sera unaoweza kusuluhisha nadharia za njama ya chuki lakini kampuni hiyo hii hatimaye ingesababisha kuondolewa kwa semi nyingi za kisiasa kupita kiasi. Bodi ina wasiwasi kuhusu ukosefu wa taarifa ambayo Meta inapaswa kushiriki kuhusu mchakato huu.
Uamuzi wa Bodi ya Usimamizi
Bodi ya Usimamizi imeunga mkono uamuzi wa Meta wa kuruhusu chapisho.
Bodi inapendekeza kwamba Meta:
- Itoe maelezo ya kina zaidi katika lugha ya Viwango vyake vya Jumuiya kuhusu Matamshi ya Chuki kuhusu jinsi inavyotofautisha majadiliano yanayohusiana na uhamiaji na matamshi ya chuki yenye madhara yanayolenga watu kulingana na hali yao ya uhamiaji. Hii inajumuisha kueleza jinsi kampuni hiyo inavyoshughulikia maudhui yanayoeneza nadharia za njama za chuki, ili watumiaji waweze kuelewa jinsi Meta inavyolinda semi za kisiasa kuhusu uhamiaji inaposhughulikia madhara yanayoweza kutokea nje ya mtandao ya nadharia hizi.
*Miuhtasari ya kesi hutoa maelezo mafupi ya kesi hizi na haina thamani ya kurejelewa katika kesi za baadaye.
Uamuzi Kamili wa Kesi
1.Muhtasari wa Uamuzi
Bodi ya Usimamizi imeunga mkono uamuzi wa Meta wa kuacha chapisha kwenye ukurasa rasmi wa Facebook wa mwanasiasa wa Ufaransa Éric Zemmour lililo na video ya Bw. Zemmour akihojiwa, ambapo anajadili mabadiliko ya kidemografia barani Ulaya na Afrika. Bodi imepata kwamba maudhui hayo hayakiuki Viwango vya Jumuiya ya Meta kuhusu Matamshi ya Chuki kwa sababu hayashambulii watu moja kwa moja kwa misingi ya sifa zilizolindwa, ikiwa ni pamoja na rangi, kabila au asili ya taifa. Wengi wa Wanabodi wamepata kwamba uamuzi wa Meta kuacha maudhui hayo kwenye Facebook unaambatana na majukumu yake ya haki za binadamu. Wanachama wachache wa Bodi wamepata kwamba sera za Meta hazitoshi katika kutimiza majukumu ya haki za binadamu ili kushughulikia tishio kubwa linalotokana na nadharia zenye madhara na za utengaji za njama kama vile Nadharia ya Ubadilishaji Mkubwa. Bodi inapendekeza kwamba Meta ieleze wazi jinsi inavyoshughulikia maudhui yanayoeleza nadharia za njama za chuki kutokana na hitaji la kulinda semi kuhusu uhamiaji inaposhughulikia uwezekano wa kutokea madhara ya nje ya mtandao kutokana na nadharia kama hizo za njama zenye madhara.
2. Maelezo na Historia ya Kesi
Mnamo tarehe 7, Julai 2023, mtumiaji alichapisha video kwenye ukurasa wa Facebook uliothibitishwa wa mwanasiasa wa Ufaransa Éric Zemmour. Katika video hiyo, ambayo ni klipu ya sekunde 50 ya mahojiano marefu zaidi yaliyofanywa kwa Kifaransa, Zemmour anajadili mabadiliko ya kidemografia barani Ulaya na Afrika. Mtumiaji aliyechapisha video alikuwa msimamizi wa ukurasa huo, uliokuwa na takriban wafuasi 300,000. Zemmour alikuwa mgombeaji katika uchaguzi wa urais wa Ufaransa mwaka 2022 na alishinda takriban 7% ya kura katika awamu ya kwanza, lakini hakuenda zaidi ya hapo. Kabla ya kugombea ofisi, Zemmour alikuwa mwandishi wa mara kwa mara katika Le Figaro na magazeti mengine, na vilevile mtoa maoni kwenye Televisheni aliyepata umaarufu kutokana na maoni yake uchokozi kuhusu dini ya Uislamu, uhamiaji na wanawake. Kama ilivyoelezwa kwa kina zaidi hapa chini, amehusika katika kesi kadhaa za kisheria na kupatikana na hatia katika baadhi yazo kwa misingi ya maoni haya. Ingawa Meta haikuzingatia mtumiaji aliyechapisha video hiyo kama mtu maarufu, kampuni hiyo haikumzingatia Zemmour kuwa mtu maarufu.
Kwenye video hiyo, Zemmour anasema kuwa: “Tangu kuanza kwa karne ya 20, idadi ya watu barani Afrika imeongezeka sana.” Anasema kwamba huku idadi ya watu barani Ulaya ikisalia katika sawa ya takriban watu milioni 400, Idadi ya watu barani Afrika imeongezeka hadi watu bilioni 1.5, “kwa hivyo mizani ya nguvu imebadilika.” Manukuu yaliyo kwa Kifaransa yanarudia madai kwenye video hiyo, kwa kusema kuwa katika miaka ya 1900 “wakati kulikuwa na Wanaulaya wanne kwa kila Mwafrika mmoja, [Ulaya] ilikuwa mkoloni wa Afrika,” na sasa “kuna Waafrika wanne kwa kila Mwanaulaya mmoja na Afrika inaikoloni Ulaya.” Takwimu hizi zinalinganishwa na takwimu zinazopatikana kutoka mashirika ya Umoja wa Mataifa zilizotolewa hapa chini. Kando na hayo, msimamo wa wengi wa Wanabodi kuhusu idadi hizi unaelezwa kwa kina katika Sehemu ya 8.2 hapa chini.
Kesi hii ilipotangazwa na Bodi mnamo tarehe 28 Novemba 2023, maudhui hayo yalikuwa yametazamwa takriban mara 20,000. Kufikia Januari 2024, maudhui hayo yalikuwa yametazamwa takriban mara 40,000 na yalikuwa na chini ya hisia 1,000 na nyingi zilikuwa za “kupendezwa,” kisha “upendo” na “Haha.”
Mnamo tarehe 9 Julai 2023, watumiaji wawili, kila mmoja kivyake waliripoti maudhui haya kuwa yanakiuka sera ya Meta dhidi ya Matamshi ya Chuki. Kampuni hiyo ilifunga ripoti zote kiotomatiki kwa sababu hazikupewa kipaumbele cha ukaguzi ndani ya kipindi cha saa 48. Meta ilieleza kwamba ripoti hupewa kipaumbele cha ukaguzi kwa njia zinazobadilika kulingana na vigezo kama vile kina cha ukiukaji unaobashiriwa, urijali wa maudhui (idadi ya mitazamo ambayo maudhui yamepata) na uwezekano kwamba maudhui hayo yatakiuka sera za kampuni hiyo. Maudhui hayo hayakuondolewa na yalisaliwa kwenye jukwaa hilo.
Mnamo tarehe 11 Julai 2023, mtumiaji wa kwanza ambaye aliripoti maudhui hayo alikata rufaa dhidi ya uamuzi wa Meta. Rufaa hiyo ilitathminiwa na mkaguzi binadamu ambaye aliunga mkono uamuzi wa kwanza wa Meta kuacha maudhui hayo. Mtumiaji aliyeripoti kisha alikata rufaa kwa Bodi ya Usimamizi.
Siku kumi kabla ya maudhui hayo kuchapishwa, tukio la kupigwa risasi vibaya kwa Nahel Merzouk, Mfaransa mwenye umri wa miaka 17 mwenye asili ya Moroko na Aljeria, ambaye alifariki baada ya polisi wawili kumpiga risasi kwa karibu viungani mwa jiji la Paris mnamo tarehe 27 Juni 2023, lilisababisha fujo na maandamano yenye vurugu nchini Ufaransa. Maandamano hayo, ambayo yalikuwa yakiendelea wakati maudhui hayo yalichapishwa, yalikuwa yalilenga kupinga vurugu za polisi na ubaguzi wa rangi wa kimfumo wa polisi nchini Ufaransa. Maandamano haya ndiyo yalikuwa ya hivi karibuni zaidi baada ya msururu mrefu wa maandamano kuhusu vurugu za polisi, ambazo, inadaiwa kuwa mara nyingi hulenga wahamiaji wenye asili ya Kiafrika na jamii nyingine zilizotengwa nchini Ufaransa.
Kulingana na Tume ya Ulaya dhidi ya Ubaguzi na Ukatili (ECRI), waathiriwa wakuu wa ubaguzi nchini Ufaransa ni wahamiaji, hususan wenye asili ya Kiafrika na nasaba zao. Mnamo 2022, Kamati kuhusu Uondoaji wa Ubaguzi wa Rangi (CERD) ilihimiza Ufaransa kuweka juhudi maradufu za kuzuia na kukabiliana na matamshi ya chuki ya ubaguzi wa rangi na kusema kwamba “licha ya juhudi za chama cha Serikali… Kamati inaendelea kuwa na wasiwasi kuhusu jinsi majadiliano ya kibaguzi yalivyokithiri na kuenea, hususan katika vyombo vya habari na kwenye intaneti.” Pia ina “wasiwasi kuhusu matamshi ya ubaguzi ya baadhi ya viongozi wa kisiasa kuhusiana na makabila fulani ya wachache, hasa Waroma, Wasafiri, Waafrika, watu wenye asili ya Kiafrika, watu wenye asili ya Uarabuni na watu wasio raia,” (CERD/C/FRA/CO/22-23, aya ya 11).
Kulingana na ripoti ya 1999 kutoka Idara ya Masuala ya Kijamii na Kiuchumi ya Muungano wa Mataifa, inakadiriwa kuwa mwaka 1900, bara la Afrika lilikuwa na watu milioni 133. Data kutoka Umoja wa Mataifa mwaka 2022 inakadiria kuwa idadi ya watu kufikia mwaka wa 2021 barani Afrika ilikuwa takriban watu bilioni 1.4. Pia inakadiria kuwa kufikia 2050, idadi inayokadiriwa ya Afrika huenda ikawa takriban watu bilioni 2.5. Kulingana na ripoti hiyo ya 1999, idadi ya watu barani Ulaya mwaka 1900 ilikuwa takriban milioni 408. Idara ya Masuala ya Kiuchumi na Kijamii ya Umoja wa Mataifa inakadiria kwamba idadi ya watu barani Ulaya mwaka 2021 ilikuwa takriban watu milioni 745 na itapungua hadi takriban milioni 716 kufikia 2050.
Nchini Ufaransa, kama ilivyo katika sehemu nyingi za dunia, kuwasili kwa idadi kubwa ya wahamiaji kutoka nchi nyingine imekuwa mojawapo ya hoja kuu za majadiliano ya kisiasa. Kufikia Septemba 2023, takriban wahamiaji 700,000 na wanaotafuta usalama walipatikana nchini Ufaransa, hii ikiifanya kuwa nchi ya tatu kwa ukubwa kati ya nchi wenyewe wa watu hawa katika Muungano wa Ulaya. Bodi ilipokuwa ikikagua kesi hii, Ufaransa ilishuhudia maandamano makubwa na majadiliano makali ya umma kuhusu uhamiaji baada ya Bunge kupitisha pendekezo jipya la sheria ya uhamiaji ambayo, miongoni mwa mambo mengine, linaweza vikomo vya uhamiaji na kukaza kanuni zinazohusu uunganishaji tena wa familia na ufikiaji wa manufaa ya kijamii. Zemmour na chama chake amekuwa katika mstari wa mbele katika majadiliano haya, akitetea vikwazo dhidi ya uhamiaji.
Zemmour amekabiliwa na kesi nyingi mahakamani na amepatikana na hatia mara kadhaa katika mahakama za Ufaransa kwa kuonyesha chuki dhidi ya rangi na kutoa maoni ya ubaguzi wa rangi katika miaka ya hivi karibuni, kutokana na taarifa yake kuhusu Waislamu, Waafrika, watu Weusi na watu wa jamii ya LGBTQIA+. Zemmour alipatikana na hatia ya uchochezi wa chuki ya ubaguzi kwa maoni aliyotoa mwaka 2011 katika televisheni ambapo alisema “wafanyabiashara wengi ni watu weusi na Waarabu. Huo ni ukweli.” Hivi karibuni zaidi, mahakama ilimpata Zemmour na hatia ya kuchochea chuki ya ubaguzi mwaka 2020 na kumpiga faini ya yuro 10,000 kwa kusema kwamba watoto wa mhamiaji ni “wezi, wauaji, ni wabakaji. Wana sifa hizo tu. Tunapaswa kuwarudisha kwao.” Ametumia na kumaliza haki zake za kukata rufaa katika kesi nyingine ambapo alipatikana na hatia na kupigwa faini na mahakama ya urekebishaji tabia kwa kuchochea ubaguzi na chuki za kidini dhidi ya jamii ya Waislamu wa Ufaransa. Hatia hiyo ilitokana na taarifa alizotoa kwenye kipindi cha televisheni mwaka 2016 kwamba Waislamu wanapaswa kupewa “chaguo kati ya Uislamu na Ufaransa” na kwamba “kwa miaka thalathini, tumekuwa tukishuhudia hali ya uvamizi, kutawaliwa (…) pia ni vita vya kufanya himaya kuwa ya kiislamu ilhali siyo, ambayo kwa kawaida ni ardhi isiyo ya kiislamu.” Mnamo Disemba 2022, Mahakama ya Ulaya ya Haki za Binadamu ilishikilia kuwa hatia hiyo haikukiuka haki ya Zemmour ya uhuru wa kujieleza.
Ingawa maudhui hayo hayataji moja kwa moja Nadharia ya Ubadilishaji Mkubwa, dhana hiyo ni muhimu katika itikadi ya kisiasa ya Zemmour na ilijitokeza sana katika kampeni yake ya urais, wakati ambapo aliahidi kuwa, iwapo angechaguliwa, kubuni “Wizara ya Kujeresha Wahamiaji Makwao.” Alitaja pia kwamba “angerudisha wageni milioni moja” makwao ndani ya miaka mitano. Kulingana na utafiti huru uliosimamiwa na Bodi, ambao ulifanywa na wataalamu wa nadharia za njama na siasa za Ufaransa, yanayovuma kwenye mitandao ya kijamii, na wanaisimu, watetezi wa Nadharia ya Ubadilishaji Mkubwa wanahoji kuwa watu weupe kutoka Ulaya wanabadilishwa kimakusudi kikabila na kitamaduni kupitia uhamiaji na ukuaji wa jamii za walio wachache. Utafiti huu unasisitiza kwamba uhamiaji unaoendelea sasa wa watu wasio weupe (na hasa Waislamu) kutoka nchi zisizo za Ulaya (wengi kutoka Afrika na Asia) kwenda Ulaya ni namna ya vita vya kidemografia. Wataalamu wa Bodi walisisitiza kwamba uhamiaji na ongezeko la uhamiaji jambo lisilopingwa kwa kweli. Badala yake, hali ya kusisitiza kwamba kuna mpango halisi au njama ya kuleta watu wasio weupe barani Ulaya ili kubadilisha au kupunguza uwiano wa idadi ya watu weupe inayofanya Nadharia ya Ubadilishaji Mkubwa kuwa njama. Wataalamu wa isimu ambao Bodi ilishauriana nayo walieleza kwamba Nadharia ya Ubadilishaji Mkubwa na maneno yanayohusiana nayo “inachochea ubaguzi wa rangi, chuki na vurugu inayolenga wahamiaji, wana Ulaya wasio weupe na kulenga Waislamu hasa.” Ripoti ya Mtandao wa Uhamasisho kuhusu Itikadi Kali ya Muungano wa Ulaya inabainisha kuwa kauli dhidi ya Wayahudi, dhidi ya Waislamu na dhidi ya uhamiaji kwa jumla zinazoenezwa na watu wanaounga mkono Nadharia ya Ubadilishaji Mkubwa zimekuwa msingi wa kuchaguliwa kwa walengwa na washambuliaji kadhaa binafsi wa hadhi ya juu barani Ulaya katika miaka ya hivi karibuni. Utafiti huo uliosimamiwa na Bodi uliashiria kuwa nadharia hii imechochea matukio kadhaa ya vurugu kote duniani katika miaka ya hivi karibuni, ikiwa ni pamoja na tukio la watu wengi kupigwa risasi katika Christchurch, Nyuzilandi, ambapo Waislamu 51 waliuawa.
Wanabodi wachache pia wanazingatia ukweli kwamba maandamano ya vurugu ya mrengu wa kulia yamekuwa yakiongezeka nchini Ufaransa katika mwaka mmoja uliopita kama muktadha muhimu. Kufuatia tukio baya la kudungwa kisu kwa kijana barobaro wakati wa mkutano wa sherehe mnamo tarehe 18 Novemba kule Crépol, jamii ya mashinani ya Ufaransa, wanaharakati na vyama vya mrengu wa kulia viliongoza maandamano ya vurugu ambapo waandamanaji walikabiliwa na polisi. Walidai kuwa wahamiaji na wachache ndio walihusika, licha ya ukweli kwamba watu tisa waliokamatwa kuhusiana na tukio la udungaji visu, wanane walikuwa Wafaransa na mmoja Mwitaliano. Waziri wa Usalama wa Ndani Gérald Darmanin alisema kwamba wanachama wa jeshi la wanamgambo “kulenga kushambulia Waarabu, watu wenye rangi tofauti ya ngozi, kunahusiana na kumbukumbu zao za Himaya ya Tatu.” Mwanasiasa wa Chama cha French Green Party Sandrine Rousseau alilinganisha maandamano haya na vurugu zinazochochewa na ubaguzi wa rangi, vurugu halisi zilizofanywa dhidi ya kabila la wachache au kikundi cha kijamii, hasa dhidi ya watu wenye asili ya Afrika Kaskazini. Tukio maarufu zaidi la vurugu zinazochochewa na ubaguzi wa rangi, ambalo mara nyingi huhusishwa na kueneza neno hilo lilifanyika mnamo tarehe 17 Oktoba 1961 wakati wa maandamano ya amani ya Waaljeria ambapo watu 200 waliuawa katika tukio la vurugu mbaya za polisi. Neno hilo limetokea mara nyingi katika miktadha tofauti nchini Ufaransa tangu wakati huo. Kwa mfano, mnamo Disemba 2022, wanasiasa wa Ufaransa walijiunga na watumiaji wa mitandao ya kijamii katika kupinga vurugu za mtaani, wakizilinganisha navurugu zinazochochewa na ubaguzi wa rangibaada ya mechi ya Kombe la Dunia kati ya Ufaransa na Moroko.
3. Bodi ya Usimamizi na Upeo
Bodi ina mamlaka ya kukagua uamuzi wa Meta kufuatia rufaa kutoka kwa mtu ambaye aliripoti hapo awali maudhui ambayo yaliruhusiwa (Kifungu cha 2 cha Mkataba, Sehemu ya 1; Sheria ndogo za Kifungu cha 3, Sehemu ya 1).
Bodi inaweza kudumisha au kubatilisha uamuzi wa Meta (Kifungu cha 3, Sehemu ya 5 ya Mkataba), na kampuni itafuata uamuzi huu (Kifungu cha 4 cha Mkataba). Meta pia lazima itathmini uwezekano wa kutekeleza uamuzi wa Bodi kuhusiana na maudhui yanayofanana yaliyo katika muktadha tofauti (Kifungu cha 4 cha Mkataba). Uamuzi wa Facebook unaweza kujumuisha mapendekezo yasiyo ya kufunga ambayo Meta lazima iyajibu (Kifungu cha 3 cha Mkataba, Sehemu ya 4); Kifungu cha 4). Wakati Meta inajitolea kushughulikia mapendekezo, Bodi hufuatilia utekelezaji wake.
4.Vyanzo vya Mamlaka na Mwongozo
Viwango vifuatavyo na kesi za awali zilikuwa msingi wa uchanganuzi wa Bodi katika kesi hii:
I.Maamuzi ya Bodi ya Usimamizi
- Kupinga Tukio la Maangamizi Makubwa
- Vurugu za Kijamii katika Jimbo la Odisha nchini India
- Katuni ya Knin
- Chapisho la Al Jazeera lililoshirikiwa
- Kusimamishwa kwa Rais wa zamani Trump
- Taswira ya Zwarte Piet
II.Sera za maudhui za Meta
Matamshi ya Chuki
Mtazamo wa sera wa Viwango vya Jumuiya kuhusu Matamshi ya Chuki unaeleza kwamba matamshi ya chuki, ambayo hufafanuliwa kama shambulio la moja kwa moja dhidi ya watu kwa msingi wa sifa zilizolindwa, hayaruhusiwi kwenye jukwaa “kwa sababu yanaweka mazingira ya vitisho na utengaji na, katika hali fulani, yanaweza kuendeleza vurugu katika ulimwengu halisi.” Sera hiyo inaorodhesha kama sifa zilizolindwa, miongoni mwa mambo mengine, rangi, ukabila, asili ya taifa na mrengu wa kidini. Sera hii inaeleza kwamba “mashambulizi yanawekwa katika viwango viwili vya kina,” huku Kiwango cha 1 kikiwa cha kina zaidi. Mtazamo wa Viwango vya Jumuiya kuhusu Matamshi ya Chuki pia unaeleza kwamba sera hiyo “hulinda wakimbizi, wahamiaji, wahamiaji kabisa na wanaotafuta usalama katika nchi za kigeni dhidi ya mashambulizi mabaya zaidi,” lakini kwamba Meta huruhusu “maoni kuhusu na usutaji wa sera za uhamiaji.” Mwongozo wa ndani wa Meta kuhusu uratibu wa maudhui unafafanua kuhusu suala hili, ukieleza kwamba unazingatia hali ya wahamiaji, wahamiaji kabisa, wakimbizi na wanaotafuta usalama katika nchi za kigeni kama isiyo ya ulinzi kamili. Hiyo inamaanisha kuwa Meta huwalinda dhidi ya mashambulizi ya Kiwango cha 1 lakini si dhidi ya mashambulizi ya Kiwango cha 2 chini ya sera ya Matamshi ya Chuki.
Sera hiyo, ambayo awali ilikuwa na viwango vitatu tofauti vya mashambulizi lakini sasa ina viwili pekee, kwa sasa inapiga marufuku kama shambulizi la Kiwango cha 2, miongoni mwa aina nyingine za maudhui “kutengwa au kubaguliwa kwa namna ya miito ya hatua, taarifa za nia, taarifa za azma au masharti, au taarifa zinazotetea au kuunga mkono zinazoelezwa kuwa: [...] ufungiaji nje wa wazi, inayomaanisha vitu kama vile kupiga marufuku vikundi fulani au kusema kwamba havirihusiwi.” Meta ilikataa ombi la Bodi la kuchapisha maelezo zaidi kuhusu mwongozo wake wa ndani kwa wakaguzi wa maudhui kuhusu hoja hii.
Katika chapisho la 2017 la Chumba cha Habari lenye kichwa “Hard Questions: Who Should Decide What Is Hate Speech in an Online Global Community?,” ambalo limeunganishwa katika sehemu ya chini ya mtazamo wa Viwango vya Jumuiya kuhusu Matamshi ya Chuki na maandishi yanayosema, “Pata maelezo zaidi kuhusu mbinu yetu ya kushughulikia matamshi ya chuki,” Meta ilitambua kuwa majadiliano ya sera kuhusu uhamiaji mara nyingi huwa “majadiliano kuhusu matamshi ya chuki, kwa kuwa pande mbili hutumia lugha ya uchochezi.” Kampuni hiyo ilisema kwamba baada ya kukagua machapisho kwenye Facebook kuhusu majadiliano ya uhamiaji kote duniani, “imeamua kubuni mwongozo mpya wa kuondoa miito ya vurugu dhidi ya wahamiaji au marejeleo yanayowadunisha — kama vile kuwalinganisha na wanyama, uvundo au uchafu.” Hata hivyo, kampuni hiyo iliruhusu “uwezo wa watu kueleza maoni yao kuhusu dhana yenyewe ya uhamiaji,” kwa sababu “inaahidi kwa dhati kufanya Facebook kusalia kuwa mahali pa majadiliano halali.”
Watu na Mashirika Hatari
Mtazamo wa Viwango vya Jumuiya kuhusu Watu na Mashirika Hatari unasema kwamba Meta hairuhusu mashirika au watu binafsi wanaokiri kushiriki katika vurugu au wanaoshiriki katika vurugu kuwa na uwepo kwenye majukwaa ya Meta. Unaeleza kwamba Meta hutathmini mashirika haya “kulingana na tabia zao mtandaoni na nje ya mtandao – kwa kina zaidi, husika kwao katika vurugu.”
Viwango vya Jumuiya kuhusu Watu na Mashirika Hatari vinaeleza kwamba Meta imepiga marufuku kuwepo kwa Mitandao ya Njama Zinazochangia Vurugu, ambazo kwa sasa zinafafanuliwa kuwa watendaji wasio wa serikali ambao: (i) “wanatambuliwa kwa jina, taarifa ya nia, ishara au maneno ya pamoja”; (ii) “huendeleza nadharia zisizo na msingi zinazojaribu kueleza sababu za matatizo makuu ya kijamii na siasa, matukio na hali kwa madai ya njama za siri za watendaji wawili au zaidi wenye nguvu”; na (iii) “wametetea kwa wazi au wamehusishwa moja kwa moja na mtindo wa madhara ya kimwili ya nje ya mtandao na wafuasi ambao wanahimizwa na nia ya kupata makini au kushughulikia madhara yanayodaiwa ambayo yametambuliwa kwenye nadharia zisizo na msingi zinazoendelezwa na mtandao huo.”
Uchanganuzi wa Bodi wa sera za maudhui pia ulitokana na dhamira ya Meta ya sauti, ambayo kampuni inafafanua kuwa “muhimu,” pamoja na maadili yake ya usalama na heshima.
III. Wajibu wa Meta wa Haki za Binadamu
Kanuni za Mwongozo wa Umoja wa Mataifa juu ya Biashara na Haki za Binadamu (UNGP), zilizoidhinishwa na Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa mnamo 2011, zina mfumo wa hiari wa majukumu ya haki za binadamu ya biashara za kibinafsi. Mnamo 2021, Meta ilitangazaSera yake ya Haki za Binadamu za Shirika, ambapo ilisisitiza tena kujitolea kwake katika kuheshimu haki za kibinadamu kwa mujibu wa UNGP. Uchambuzi wa Bodi wa wajibu wa Meta kwa haki za binadamu katika kesi hii ulitokana na viwango vifuatavyo vya kimataifa:
- Haki ya uhuru wa kujieleza: Kifungu cha 19, Mkataba wa Kimataifa kuhusu Haki za Kiraia na Siasa ( ICCPR), Kifungu cha 20, aya ya 2, ICCPR, Maoni ya Jumla Nambari 34, Kamati ya Haki za Binadamu, 2011; Mjumbe Maalum wa Umoja wa Mataifa (UNSR) kuhusu uhuru wa maoni na kujieleza, anaripoti: A/HRC/38/35 (2018) na A/74/486 (2019).
- Usawa na kutobagua: Kifungu cha 2, aya ya 1 na Kifungu cha 26, ICCPR; Kifungu cha 2, Mkataba wa Kimataifa kuhusu Kuondoa Namna Zote za Ubaguzi wa Rangi ( ICERD); Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa, uamuzi A/RES/73/195.
- Haki ya kuishi: Kifungu cha 6, ICCPR.
5. Mawasilisho ya Mtumiaji
Bodi ilipokea mawasilisho kutoka kwa mtumiaji ambaye aliripoti maudhui hayo na kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa Meta ili kuyaacha, kama sehemu ya rufaa yake kwa Bodi. Katika wasilisho hilo, mtumiaji anayekata rufaa anasema kwamba Zemmour anaeleza ukoloni na uhamiaji kuhusiana na idadi ya watu kupitia kiasi pekee, hali ambayo mtumiaji aliainisha kama “habari za uongo.”
6. Mawasilisho ya Meta
Baada ya Bodi kuchagua kesi hii, Meta ilikagua chapisho hili kwa kulilinganisha na sera dhidi ya Matamshi ya Chuki pamoja na wataalamu wa mada husika na kubaini kuwa uamuzi wake wa awali wa kuyaacha maudhui hayo ulikuwa sahihi. Meta haikutoa maelezo zaidi kuhusu masuala mahususi ya ujuzi wa wataalamu waliokuwa wakifanya ukaguzi huu wa ziada. Meta ilisisitiza kwamba, ili maudhui fulani yachukuliwe kuwa ya ukiukaji, sera inahitaji kikundi cha sifa iliyolindwa na shambulio la moja kwa moja – na kwamba madai kuhusu mabadiliko ya idadi ya watu na ukoloni hayakuwa na vipengee hivyo. Meta alieleza kwamba haizingatii madai kwamba kikundi kimoja kina “ukoloni” juu ya mahali ili iwe shambulizi lenyewe ilimradi haijumuishi mwito wa kutengwa, na ilisisitiza kwamba “inataka kuruhusu wananchi ili kujadili sheria na sera za nchi yao ilimradi majadiliano hayo si mashambulizi dhidi ya vikundi vilivyo hatarini ambayo wanaweza kuwa wanasimamiwa na sheria hizo.” Hatimaye, Meta ilieleza kwamba maudhui hayo hayatambui kikundi chenye sifa iliyolindwa kwa sababu Zemmour anarejelea “Afrika,” bara na nchi zilizomo, na kwamba “sera dhidi ya Matamshi ya Chuki hailindi nchi au taasisi dhidi ya mashambulizi.”
Meta ilikataa kuondoa usiri unaohusiana na mchakato wa uundaji wa sera ya kampuni hiyo dhidi ya nadharia za njama zenye madhara. Badala yake Meta ilisema: “Tumezingatia chaguo za sera mahususi kwa maudhui yanayojadili nadharia za njama ambazo vinginevyo hazikiuki sera zetu zilizopo. Hata hivyo, tumehitimisha kwamba, kwa sasa, utekelezaji wa chaguo zozote ungesababisha hatari ya kuondolewa kwa kiasi kikubwa cha kauli za kisiasa.”
Bodi iliuliza Meta maswali nane katika maandishi. Maswali hayo yalihusu uundaji wa sera za Meta kuhusiana na Nadharia ya Ubadilishaji Mkubwa; uwezo wa kutekelezwa kwa mikondo mbalimbali ya sera ya Dhidi ya Matamshi ya Chuki pamoja na Watu na Mashirika Hatari; na historia ya ukiukaji kwa ukurasa wa Facebook na uchapishaji wa mtumiaji. Meta ilijibu maswali sita ya Bodi, huku maswali mawili yakikosa kujibiwa ipasavyo. Baada ya Meta kukosa kutoa maelezo ya kutosha ya kujibu swali ya awali la Bodi kuhusu uundaji wa sera kuhusiana na Nadharia ya Ubadilishaji Mkubwa, Bodi iliuliza swali la kufuatilia ambalo Meta ilitoa maelezo ya ziada ila bado hayakuwa tondoti vya kutosha.
7.Maoni ya Umma
Bodi ya Usimamizi ilipokea maoni 15 ya umma. Maoni saba yaliwasilishwa kutoka Marekani na Kanada, matatu kutoka Ulaya, mawili kutoka Asia ya Kati na Kusini, moja kutoka Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini, moja kutoka Asia Pasifiki na Oceania na moja kutoka Kusini mwa Jangwa la Sahara. Jumla hii inajumuisha maoni ya umma ambayo yalikuwa yakijirudia au yaliwasilishwa kwa idhini ya kuchapisha lakini hayakutimiza masharti ya Bodi ya uchapishaji. Maoni ya umma yanaweza kuwasilishwa kwa Bodi kwa ridhaa au bila ridhaa ya kuchapisha, na kwa ridhaa au bila ridhaa ya kupata sifa (yaani., bila kutambulishwa).
Mawasilisho yalishughuliki mada mbili kuu. Kwanza, maoni mengi yalisisitiza kwamba kuomba maudhui yaliyokuwa yakikaguliwa katika kesi hii ilikuwa ni udhibiti, na hata “ingefanya kuongezeka kwa hasira ya wananchi wanaohisi kuwa sauti zao hazitasikilizwa,” (PC-22009). Pili, mashirika mawili yaliwasilsha maoni yakisisitiza athari mbaya ya nje ya mtandao ya aina hii ya maudhui na, hususan, Nadharia ya Ubadilishaji Mkubwa. Maoni yote mawili yalihoji kuwa kulikuwa na uhusiano katika ya mauaji ya wengi katika kanisa la Christchurch na nadharia (PC-22013, Wakfu wa Digital Rights; PC-22014, Global Project Against Hate na Extremism).
Ili kusoma maoni ya umma yaliyowasilishwa kuhusu kesi hii, tafadhali bofya hapa.
8.Uchanganuzi wa Bodi ya Usimamizi
Bodi ilichanganua sera za maudhui ya Meta, maadili na wajibu wa haki za binadamu ili kubaini iwapo maudhui katika kesi hii yanafaa kuondolewa. Bodi pia ilitathmini athari za kesi hii kwa mtazamo mpana wa Meta wa usimamizi wa maudhui.
Bodi ilichagua kesi hii kama fursa ya kukagua mbinu ya Meta ya kushughulikia maudhui yanayolenga wahamiaji katika muktadha wa semi zinazoongezeka kote duniani dhidi ya uhamiaji, na majadiliano makali ya umma kuhusu sera za uhamiaji; hususan kutokana na changamoto zinazohusishwa na kutofautisha maudhui yenye madhara kwa wingi na kauli za kisiasa zinazojadili sera za uhamiaji.
8.1 Utiifu wa Sera za Maudhui za Meta
Bodi inahitimisha kwamba maudhui hayo hayakiuki sera za Meta. Kwa hivyo, uamuzi wa Meta wa kuacha maudhui hayo kwenye Facebook ulikuwa sahihi. Hata hivyo, wanabodi wachache wanaamini kuwa, sera za Meta zingetofautisha kwa wazi usutaji mkali hata zaidi wa sera za uhamiaji na usemi unaohusika katika nadharia za njama ambazo zina madhara kwa vikundi vyenye sifa iliyolindwa.
I.Kanuni za Maudhui
Matamshi ya Chuki
Wengi wa Bodi walihitimisha kwamba maudhui katika kesi hii hayakiuki Viwango vya Jumuiya ya Meta kuhusu Usemi wa Chuki, na kwa kweli, mfano wa maoni yaliyolindwa ingawa yenye utata kuhusu mada ya uhamiaji. Klipu ya sekunde 50 ya mahojiano na Zemmour iliyochapishwa na mtumiaji hayana mwito wa vurugu, wala haishushi hadhi moja kwa moja au kutumia lugha ya chuki kwa vikundi vilivyo katika hatari. Ukweli kwamba Zemmour hapo awali alikuwa amefunguliwa mashtaka na kupatikana na hatia ya kutumia lugha ya chuki au kwamba mada za chapisho hilo zinafanana na zile Nadharia ya Ubadilishaji Mkubwa – ambayo wengi wanaamini kuwa inachochea vurugu dhidi ya wahamiaji na wanachama wa makundi ya wachache – si sababu tosha ya kuondoa chapisha ambalo halijakiuka viwango vya Meta. Sera hiyo inataka vipengee viwili viwepo ili maudhui yazingatiwe kuwa ya ukiukaji: (i) “shambulizi la moja kwa moja” na (ii) kikundi chenye “sifa iliyolindwa” kinacholengwa na shambulizi hilo la moja kwa moja. Meta inafafanua “mashambulizi ya moja kwa moja” kama, miongoni mwa semi nyingine, “utengaji au ubaguzi kwa namna ya miito ya hatua,” kama ilivyoelezwa kwa kina chini ya Sehemu ya 4 hapo juu. Zaidi ya hayo, mtazamo wa sera unabainisha wazi kwamba Meta huruhusu “maoni kuhusu na usutaji wa sera za uhamiaji.”
Kwa wengi, maoni ya Zemmour kwenye video hiyo yanalenga sana maelezo ya kidemografia anayowasilisha kuhusu Afrika, Ulaya na “ukoloni.” Video hiyo ina, miongoni mwa mambo mengine, taarifa, “Kwa hivyo mizani ya nguvu imebatilishwa,” na “Wakati sasa kuna Waafrika wanne kwa kila Mwanaulaya mmoja, nini hufanyika? Afrika inatawala Ulaya, na hasa, Ufaransa.” Maoni ya Zemmour hayana shambulio lolote la moja kwa moja na kwa kweli hatumii kauli “Ubadilishaji Mkubwa”au kurejelea moja kwa moja nadharia hiyo. Hakuna mwito wa moja kwa moja wa kutenga kikundi chochote barani Ulaya, wala taarifa yoyote kuhusu inayoweza kuainishwa kama kasumba mbaya, maneno ya kudhalilisha au shambulizi lolote lingine la moja kwa moja. Hata hivyo, Bodi ina wasiwasi kwamba Meta haizingatii Waafrika kama kikundi chenye sifa iliyolindwa, kutokana na ukweli kwamba asili ya taifa, rangi na dini ni sifa zinazolinda chini ya sera za Meta na sheria ya kimataifa ya haki za binadamu. Waafrika wametajwa kote kwenye maudhui hayo. Afrika ni bara lililo na mataifa mengi – hivyo “Waafrika” inarejelea watu ambao ni raia ya nchi za Afrika. Pili, katika muktadha wa maoni ya Zemmour na majadiliano kuhusu uhamiaji nchini France, neno “Waafrika” pia linawaafiki kuwafafanua Waafrika wasio weupe, hususan Waafrika Weusi na Waislamu.
Watu na Mashirika Hatari
Wengi wa Wanabodi pia walihitimisha kwamba maudhui hayo hayakiuki sera ya Meta dhidi ya Watu na Mashirika Hatari, kutokana na kukosa vipengee vinavyohitajika ili kutathmini maudhui haya kama sehemu ya Mtandao mpana wa Nadharia Inayosababisha Vurugu.
Kama ilivyoelezwa chini ya Sehemu ya 6 hapa juu, Meta ilizingatia chaguo za sera mahususi kwa maudhui yanayojadili nadharia za njama ambazo vinginevyo hazikiuki sea zozote lakini ilihitimisha kwamba, kwa sasa utekelezaji wa chaguo zozote ungesababisha kuondolewa kwa kiasi kikubwa cha kauli za kisiasa. Bodi inaeleza wasiwasi wake kuhusu ukosefu wa taarifa kutoka Meta katika kujibu maswali ya Bodi kuhusu mchakato huu wa uundaji wa sera. Bodi imebainisha kuwa kampuni hiyo haikutoa taarifa zozote mahususi kuhusu utafiti ambao ilifanya, maelezo yaliyokusanywa, upeo wa ufikio wake, aina za wataalamu waliopata ushauri wao wala chaguo tofauti za sera ambazo ilichambua. Bodi pia ina wasiwasi kwamba Meta ilichagua kutoshiriki taarifa kuhusu mchakato wa uundaji wa sera na matokeo yake kwa umma.
Wachache wa Bodi wanaelewa kwamba licha ya kwa maudhui inalenga kwa njia isiyo ya moja kwa moja vikundi kadhaa vinavyolandana vyenye sifa iliyolindwa (Watu weusi, Waarabu na Waislamu), kama maneno yake yalivyotumiwa kwa sasa, kanuni zilizopo kwenye sera dhidi ya Matamshi ya Chuki pamoja na Watu na Mashirika Hatari hazipigi marufuku maudhui kama haya. Ukweli kwamba chapisho hilo linarudia tu sehemu “nzuri” tu za Nadharia ya Ubadilishaji Mkubwa haifanyi uamuzi wowote. Katika uamuzi wa Bodi kuhusu kesi ya Kusimamishwa kwa Rais wa Zamani Trump, “ni lazima Facebook ichunguze machapisho ya watumiaji wenye ushawishi kwa muktadha kulingana na njia ambayo wanaweza kueleweka, hata ikiwa ujumbe wao wa kuchochea unatumia lugha iliyoundwa kuepuka uwajibikaji.”
Licha ya hayo, kama ilivyoelezwa kwa kina zaidi katika Sehemu ya 8.3, kwa wachache wa Bodi, mbinu ya Meta ya kushughulikia maudhui yanayoeneza nadharia za njama zenye madhara, kama vile Nadharia ya Ubadilishaji Mkubwa, inalingana na malengo ya sera tofauti ambayo kampuni hiyo imebainisha ili kuzuia uundaji wa mazingira ya vitisho na kutenga yanayoathiri wachache wanaolindwa dhidi ya madhara ya mtandaoni na ya nje ya mtandao. Ingawa wengi wa Bodi wanakubaliana sana kwamba sera za Meta zinapaswa kuruhusu usutaji na majadiliano ya masuala yote (kama vile uhamiaji) yanayofaa katika jamii zenye demokrasia, pia wanapaswa kuweka vidhibiti vya wazi vya kuzuia kuenea kwa mashambulizi yasiyo ya moja kwa moja au ya moja kwa moja dhidi ya vikundi vilivyo hatarini, kwa kuzingatia madhara ya nje ya mtandao ya dhana fulani za njama, kama vile Nadharia ya Ubadilishaji Mkubwa.
II. Uwazi
Meta hutoa maarifa fulani kuhusu jinsi ya kushughulikia maudhui yanayohusiana na uhamiaji katika Kituo chake cha Uwazi chini ya Viwango vya Jumuiya kuhusu Matamshi ya Chuki ambapo kampuni hiyo inaelezwa kwamba wakimbizi, wahamiaji, wahamiaji kabisa na wanaotafuta usalama katika nchi za kigeni wanalindwa dhidi ya mashambulizi mengi mabaya. Katika chapisho la 2017 la Chumba cha Habari, lililounganishwa kutoka mtazamo wa sera wa Matamshi ya Chuki, Meta inatoa maelezo kadhaa ya ziada. Hata hivyo, kampuni hiyo haielezi moja kwa moja jinsi inavyoshughulikia maudhui yanayohusiana na Nadharia ya Ubadilishaji Mkubwa. Chapisho hilo la 2017 lina taarifa zinazofaa za mada lakini halikusasishwa baada ya mchakato wa uundaji wa sera wa 2021 uliotajwa chini ya Sehemu ya 6 hapo juu. Meta pia haielezi moja wa moja kwenye sera yake inayopatikana kwa umma kwamba miito ya kutengwa inaruhusiwa katika muktadha wa majadiliano kuhusu uhamiaji. Pia, si wazi jinsi mashambulizi yasiyo ya moja kwa moja au yaliyofichwa katika muktadha huu yanavyoshughulikiwa.
8.2 Utiifu wa Wajibu wa Haki za Binadamu wa Meta
Wengi wa Wanabodi wamepata kuwa kuacha maudhui hayo kunaambatana na majukumu ya Meta ya haki za binadamu. Wachache wanaamini kwamba , ili kuambatana na wajibu wake wa haki za binadamu, Meta inahitaji kubadilisha sera zake ili huduma zake zisitumiwe vibaya na watu wanaoendeleza nadharia za njama zinazosababisha madhara ya mtandaoni na ya nje ya mtandao.
Uhuru wa Kujieleza (Kifungu cha 19 cha ICCPR)
Kifungu cha 19 cha ICCPR kinatoa ulinzi mpana wa haki za uhuru wa kujieleza, ikiwa ni pamoja na “uhuru wa kutafuta, kupokea na kupokezana taarifa na mawazo ya aina zote,” ikiwa ni pamoja na “mijadala ya kisiasa” na maoni kuhusu “masuala ya umma,” (Maoni ya Jumla Nambari. 34, aya ya 11). Kamati ya Haki za Binadamu imesema kwamba upeo wa haki hii “unaruhusu hata usemi unaoweza kuchukuliwa kuwa ya kuudhi sana, ingawa usemi kama huo unaweza kuzuiwa kwa mujibu wa kanuni za kifungu cha 19, aya ya 3 na kifungu cha 20” ili kulinda haki au hadhi ya watu wengine au kupiga marufuku uchochezi wa ubaguzi, ukatili au vurugu (Maoni ya Jumla Nambari 34, aya ya 11).
Katika muktadha wa majadiliano ya umma kuhusu uhamiaji, Mkutano wa Pamoja wa Umoja wa Ulaya ulibainisha kujitolea kwake “kulinda uhuru wa kujieleza kwa mujibu wa sheria za kimataifa, kutambua kuwa mjadala huru na wazi unachangia katika uelewa tondoti wa vipengee vyote vya uhamiaji.” Pia imeendelea kujitolea “kuendelea majadiliano ya umma ambayo ni wazi yenye misingi ya ushahidi kuhusu uhamiaji na wahamiaji kwa ushirikiano na sehemu zote za jamii zinazozalisha dhana ya kweli, utu na ya manufaa kuhusiana na suala hili,” (A/RES/73/195, aya ya 33). Uhamiaji na sera zinazohusiana – zinazopingwa sana na zinazofaa katika michakato ya kisiasa si tu nchini Ufaransa bali katika kiwango cha kimataifa – ni mada halali za mjadala kwenye majukwaa ya Meta. Kwa wengi wa Wanabodi, kutokana na athari zinazoweza kuwepo za majadiliano ya umma, kupiga marufuku aina hii ya usemi kwenye majukwaa ya Meta kunaweza kuwa ukiukaji wa wazi wa huru wa kujieleza na mfano hatari. Kwa Wanabodi wachache, ni hasa kwa sababu ya majadiliano ya wazi na ya misingi ya ushahidi kuhusu uhamiaji ni muhimu sana katika jamii yenye demokrasia, hivi kwamba kuenea kwa nadharia za njama, kama vile Nadharia ya Ubadilishaji Mkubwa, katika majukwaa ya mitandao ya kijamii inaweza kuwa na madhara makubwa. Kama ilivyoripotiwa na taasisi ya Strategic Dialogue, mbinu zinazotumiwa za kutangaza nadharia hiyo “ni pamoja na picha za meme za ubaguzi wa rangi zinazoshusha hadhi, kuharibu na kuwakilisha visivyo data ya kidemografia na kutumia sayansi isiyo na misingi ya ushahidi.”
Ambapo serikali imeweka vikwazo dhidi ya usemi, vikwazo hivyo lazima vitimize masharti ya kutii sheria, lengo halali na umuhimu na ulinganifu (Kifungu cha 19, aya ya 3 ya ICCPR). Masharti haya mara nyingi huitwa “jaribio la sehemu tatu.” Bodi hutumia mfumo huu kutafsiri ahadi za hiari za haki za binadamu za Meta, kuhusiana na uamuzi wa maudhui ya mtu binafsi unaokaguliwa na kile kinachosemwa na Meta kuhusu usimamizi wa maudhui. Kama vile Mjumbe Maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu uhuru wa kujieleza alivyosema, ingawa “kampuni hazina wajibu wa Serikali, aina ya athari zao huzihitaji kutathmini aina sawa ya maswali kuhusu kulinda hali za kujieleza huru za watumiaji wao,” ( A/74/486, aya ya 41).
I. Uhalali (uwazi na upatikanaji wa sheria)
Kanuni ya uhalali inahitaji sheria zinazowekea kikomo usemi kuweza ziwe zinaweza kufikiwa na ziwe wazi, ziundwe kwa usahihi wa kutosha ili kuwezesha mtu binafsi kudhibiti tabia zake ipasavyo (Maoni ya Jumla Nambari 34, aya ya 25). Isitoshe, huenda kanuni hizi “haziwezi kutoa uamuzi usiozuiliwa kwa kizuizi cha uhuru wa kujieleza kwa wale walioshtakiwa kwa utekelezaji [wao]” na lazima “zitoe mwongozo wa kutosha kwa waliohukumiwa na utekelezaji wao ili kuwawezesha kuwa na uhakika kuhusu aina za usemi zimewekewa kikomo vizuri na aina zisizo na kikomo” ( Ibid). Ilitumika kwa sheria zinazosimamia matamshi ya mtandaoni, Mwandishi Maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu uhuru wa kujieleza amesema zinapaswa kuwa wazi na mahususi ( A/HRC/38/35, aya ya 46). Watu wanaotumia majukwaa ya Meta wanapaswa kufikia na kuelewa sheria na wakaguzi wa maudhui wanapaswa kuwa na mwongozo wazi kuhusu utekelezaji wao.
Hamna sera zozote za Meta za sasa ambazo zinapiga marufuku kwa njia “mahususi na kwa uwazi” maudhui katika kesi hii. Kwa wengi wa Wanabodi, mtumiaji wa kawaida, anayesoma Viwango vya Jumuiya kuhusu Matamshi ya Chuki au chapisho la blogu la Meta la 2017 la “Hard Questions” (lililounganishwa kutoka kwenye Viwango vya Jumuiya) huenda akapata taswira kwamba mashambulizi mabaya zaidi dhidi ya wahamiaji kabisa na wahamiaji ndio yanaweza kuondolewa, kwa kuwa Meta inaashiria kuwa inataka kuruhusu maoni na usutaji wa sera za uhamiaji kwenye majukwaa yake. Wengi wa Wanabodi wamepata kuwa ahadi hii inaambatana na wajibu wa Meta wa haki za binadamu. Kwa wengi, sera dhidi ya Matamshi ya Chuki inalenga kuzuia uundaji wa mazingira ya utendaji au ubaguzi ambayo inachangiwa na nadharia za njama zenye madhara kama vile Nadharia ya Ubadilishaji Mkubwa. Kwa kuwa maudhui yanayohusiana na nadharia kama hizo hulenga vikundi vilivyo hatarini na vya wachache na ni sehemu ya shambulizi dhidi ya hadhi yao, watumiaji wa kawaida wanaweza kutarajia ulinzi dhidi ya aina hii ya maudhui chini ya sera ya Meta dhidi ya Matamshi ya Chuki.
Sera ya sasa ya Meta dhidi ya Watu na Mashirika Hatari haina kanuni zozote zinazopiga marufuku maudhui katika kesi hii. Kwa wengi, hata ikiwa Meta itapiga marufuku kwa njia mahususi na wazi maudhui yanayohusu Nadharia ya Ubadilishaji Mkubwa kwenye majukwaa yake, maudhui katika kesi hii hayajafika kiasi cha kutaja nadharia au kueleza vipengele vya nadharia hiyo kwa namna inayoweza kuzingatiwa kuwa ya njama au yenye madhara. Chapisho hilo halidai kuwa mitiririko ya uhamiaji kuingia Ulaya inayohusisha vikundi mahususi vya watu ni sehemu ya njama ya siri inayohusisha watendaji wenye nia fiche.
II.Lengo Halali
Uzuiaji wowote wa uhuru wa kujieleza unafaa pia kufuatilia angalau mojawapo ya malengo halali yaliyoorodheshwa katika ICCPR, ambayo yanajumuisha kulinda “haki za wengine.” “Neno ‘haki’ inajumuisha haki za binadamu kama ilivyotambuliwa kwenye Mkataba na kwa jumla zaidi katika sheria za kimataifa za haki za binadamu,” ( Maoni ya Jumla Nambari 34, aya ya 28).
Katika maamuzi kadhaa, Bodi imegundua kwamba sera ya Meta dhidi ya Matamshi ya Chuki, ambayo inalenga kuwalinda watu dhidi ya madhara yanayosababishwa na matamshi ya chuki, ina lengo halali linalotambuliwa na viwango vya kimataifa vya sheria za haki za binadamu (angalia, uamuzi wa Katuni ya Knin). Inalinda haki ya kuishi (Kifungu cha 6, aya ya 1, ICCPR) pamoja na haki ya usawa na kutobagua, ikijumuisha kulingana na rangi, kabila na asili ya taifa (Kifungu cha 2, aya ya 1, ICCPR; Kifungu cha 2 ICERD. Awali Bodi ilibaini kuwa sera ya Meta dhidi ya Watu na Mashirika Hatari inalenga kuzuia na kukatiza madhara halisi kwa lengo halali la kulinda haki za wengine (angalia uamuzi wa Chapisho Lililoshirikiwa la Al Jazeera). Hata hivyo, Bodi imerudia kubainisha kuwa si lengo halali kuzuia watu kujieleza kwa madhumuni pekee ya kulinda watu dhidi ya maelezo ya kuudhi (angalia Taswira ya Zwarte Piet inayotaja Ripoti ya Mjumbe Maalum wa Umoja wa Ulaya kuhusu uhuru wa kujieleza, ripoti A/74/486, aya ya 24 na Kusimamishwa kwa Rais wa Zamani Trump), kwa kuwa sheria ya haki za kimataifa za binadamu iliweka thamani ya juu kwa kujieleza bila kuzuiwa (Maoni ya Jumla Nambari 34, aya ya 38).
III. Umuhimu na Uwiano
Kanuni ya umuhimu na usawa inatoa vizuizi vyovyote vya uhuru wa kujieleza “lazima viwe vinafaa ili kufanikisha kazi yao ya ulinzi; lazima viwe ni vyombo vya ukali wa chini zaidi kati ya vile vinavyoweza kufikia lengo lao la ulinzi; [na] lazima viwe na usawa na mapendeleo ya kulindwa,” ( Maoni ya Jumla Nambari 34, aya ya 34). Asili na aina za majibu zinazopatikana kwa kampuni kama vile Meta ni tofauti na zinazopatikana kwa Serikali, na mara nyingi huwakilisha ukiukaji wa haki wenye athari ndogo ikilinganishwa na, kwa mfano, adhabu za uhalifu. Kama sehemu ya wajibu wao wa haki za binadamu, kampuni za mitandao ya kijamii zinapaswa kuzingatia aina mbalimbali za majibu yanayowezekana kwa maudhui yenye matatizo ambayo hayawezi kufutwa ili kuhakikisha kuwa vizuizi vinapunguzwa ( A/74/486 aya ya 51).
Wakati wa kutathmini hatari zinazosababishwa na maudhui ya vurugu, Bodi inaongozwa na jaribio lenye sehemu sita lililoelezwa katika Mpango wa Hatua wa Rabat, ambalo linashughulikia uchochezi wa ubaguzi, ukatili au vurugu (OHCHR, A/HRC/22/17/Kiambatisho cha 4, 2013). Jaribio hilo linazingatia muktadha, mzungumzaji, nia, maudhui na mtindo, kiasi cha kusambazwa kwa usemi na uwezekano wa kutokea madhara.
Kwa Wanabodi wengi, hatua ya kuondoa maudhui katika kesi hii si muhimu wala haina uwiano. Jaribio la Rabat linasisitiza maudhui na mtindo wa kauli kuwa “kipengele muhimu cha uchochezi.” Katika maudhui yanayoangaziwa kwenye kesi hii, maoni ya Zemmour, kama yalivyozalishwa tena katika klipu ya sekunde 50 iliyochapishwa na mtumiaji, hayahusiana moja kwa moja na vipengee vya njama vya Nadharia ya Ubadilishaji Mkubwa na video hiyo haina vipengee vya uchochezi, kama vile picha za vurugu au za uchochezi. Maoni na manukuu pia hana miito yoyote ya moja kwa moja ya vurugu au utengaji. Wengi wanaamini kuwa ingekiuka uhuru wa kujieleza kutojumuisha maudhui ya siasa yenye utata kwa msingi wa kauli zinazotolewa na mzungumzaji kwingineko. Wengi wanatazama idadi zilizotajwa na Zemmour kuwa ambazo zimepigwa chuku kiasi. Wengi pia wanabainisha kuwa suala kuu la kauli ya Zemmour kwenye video ni uhamiaji, pengine mojawapo ya masuala makuu ya siasa za leo.
Kwa wengi wa Wanachama wa Bodi, maudhui katika kesi hii hayakiuki sera za sasa za Meta (angalia Sehemu ya 8.1). Hata hivyo, kampuni imebainisha mkusanyiko wa sera zinazolenga kuzuia uundaji wa mazingira ya utengaji na vitisho ambayo yanaathiri tu wachache wanaolindwa mtandaoni (kuathiri sauti za vikundi vilivyotengwa) lakini pia nje ya mtandao. Chini ya sera hizi, dhana dhidi ya wayahudi na ubabe wa watu weupe, pamoja na ma kutoka kwenye Mitandao ya Njama Zinazosababisha Vurugu hudhibitiwa. Kuondoa maudhui kama hayo kunaendana na wajibu wa Meta wa haki za binadamu. Kama ilivyoelezwa katika sehemu ya 2 hapo juu, Nadharia ya Ubadilishaji Mkubwa inahoji kuwa kuna njama inayokusudiwa ya kubadilisha na watu wenye asili ya Afrika na Asia kuchukua nafasi ya watu weupe barani Ulaya. Kuenezwa kwa dhana za Nadharia ya Ubadilishaji Mkubwa kumechangia uchochezi wa ubaguzi wa rangi, chuki na vurugu zinazolenga wahamiaji, Wanaulaya wasio weupe na Waislamu. Wanabodi wachache wanasisitiza kuwa si tu wazo dhahania au maoni yenye utata bali ni nadharia ya njama ya kawaida ambayo husababisha madhara ya mtandaoni na ya nje ya mtandao. Bila shaka, inachangia katika uundaji wa mazingira ya utengaji na vitisho kwa baadhi ya watu wachache. Ushahidi wa madhara uliotolewa na kupitia ujumuishaji, uongezaji na usambazaji wa kwa kasi wa maudhui dhidi ya wayahudi kwenye majukwaa ya Meta, kama ilivyojadiliwa katika kesi ya Kupinga Tukio la Maangamizi Makubwa, ni sawa na ushahidi wa madhara unaotolewa na Nadharia ya Ubadilishaji Mkubwa, inayoashiriwa chini ya Sehemu ya 2. Kwa sababu hizi, wengi walipata haiambatani na kanuni ya kutobagua na maadili ya Meta ya usalama na heshima ambayo Meta imeamua kulinda vikundi fulani vilivyotishiwa dhidi ya utengaji na ubaguzi unaosababishwa na dhana za njama, huku ikiacha wengine walio katika hali sawa na hiyo ya hatari bila kuwalinda. Wanabodi wachache hawakupata sababu ya kutosha ya kutofautisha mbinu ya Meta ya kushughulikia Nadharia ya Ubadilishaji Mkubwa na mbinu ya kampuni hiyo ya kushughulikia dhana nyingine za njama zilizotajwa hapa juu, ambayo Meta inaratibu kwa mujibu wa wajibu wake wa haki za binadamu.
Suala linalohusiana na lililo hapo juu, wachache wa Wanabodi, changamoto kubwa zaidi ambalo kampuni za mitandao ya kijamii inakabiliana nayo si vipande vya maudhui, lakini katika kukusanya maudhui hatari yanayoshirikiwa kwa kiwango kikubwa na kwa kasi ya juu. Bodi ilieleza kuwa “uratibu wa maudhui ili kushughulikia madhara ya jumla ya usemi wa chuki, hata pale ambapo kujieleza huko hakuchochei vurugu wala ubaguzi, kunaweza kuambatana na wajibu wa Facebook wa haki za binadamu katika hali fulani.” (angalia maamuzi ya Taswira ya Zwarte Piet na Vurugu za Jamii katika Jimbo la Odisha nchini India). Mnamo 2022, CERD ilionyesha wasiwasi wake “kuhusiana na jinsi mijadala ya ubaguzi wa rangi na ubaguzi ilivyoendelea na kuenea nchini Ufaransa, hususan katika vyombo vya habari na kwenye Intaneti.” Kwa wachache, kuongezeka kwa maudhui yanayohusiana na Nadharia ya Ubadilishaji Mkubwa “kunaweka mazingira ambapo vitendo vya vurugu vina uwezekano zaidi wa kuruhusiwa na kuendeleza ubaguzi katika jamii,” (angalia maamuzi ya Taswira ya Zwarte Piet na Vurugu za Jamii katika Jimbo la Odisha nchini India). Wachache wanaangazia kuwa, chini ya UNGP, “biashara zinapaswa kuwa waangalifu kabisa kwa athari zozote za haki za binadamu kwa watu binafsi kutoka katika vikundi au watu ambao wanaweza kuwa katika hatari kubwa ya kuathirika na kutengwa,” (UNGPs, Kanuni za 18 na 20). Kama ilivyotajwa katika Sehemu ya 2 hapo juu, waathiriwa wakuu wa ubaguzi nchini Ufaransa ni wahamiaji, hususan wenye asili ya Kiafrika na nasaba zao. Katika mahojiano ya 2023, Mkurugenzi Mkuu wa Usalama wa Ndani wa Ufaransa alishiriki imani yake kwamba vikundi vya kigaidi, ikiwa ni pamoja na vinavyofikiri kuwa ni lazima vichukue hatua ili kukomesha “Ubadilisha Mkubwa” vinawakilisha tishio kubwa kwa taifa.
Ingawa Meta ilisema kwamba kudhibiti maudhui yanayohusiana na nadharia ya njama kunaweza kusababisha hatari ya kuondolewa “kiasi kisichokubalika cha kauli za kisiasa,” Wanabodi wachache walisema kuwa kampuni hiyo haikutoa ushahidi wala data yoyote kama ushahidi wa hayo. Zaidi ya hayo, Meta haikueleza kwa nini hali ni hivi kuhusiana na maudhui ya Nadharia ya Ubadilishaji Mkubwa lakini si, kwa mfano, maudhui ya ubabe wa watu weupe au dhidi ya wayahudi, kwa kuwa haya pia yanaeleweka kama kueneza nadharia za njama. Kutokana sababu zilizo hapo juu, kwa wachache, Meta inahitaji kukagua sera zake ili kushughulikia maudhui yanayoendeleza Nadharia ya Ubadilishaji Mkubwa, isipokuwa kampuni hiyo iwe na ushahidi wa kutosha: (i) kuondoa maudhui yanayotokana na kuenezwa kwa aina hii ya maudhui, kama inavyojadiliwa katika uamuzi huu; au (ii) kuonyesha kwamba athari ya kuratibu aina hii ya maudhui kwa kauli inayolindwa ya kisiasa haina uwiano. Kwa jibu linalowiana, miongoni mwa chaguo nyingine, Meta ingezingatia kuunda sera ya mapendekezo pekee ili kuruhusu uondoaji wa maudhui yanayounga mkono Nadharia ya Ubadilishaji Mkubwa kwa njia bayana, bila kuathiri kauli zinazolindwa za kisiasa, au kuzingatia watendaji waliobainishwa moja kwa moja wanaojihusisha katika Nadharia ya Ubadilishaji Mkubwa kama sehemu ya Mtandao wa Njama ya Kuchochea Vurugu chini ya sera ya Meta dhidi ya Watu na Mashirika Hatari.
Wengi wana shauku kwamba sera yeyote inaweza kuundwa ambayo chini yake maudhui haya yangekuwa ya ukiukaji, hali ambayo ingetimiza masharti ya uhalali, umuhimu na uwiano, hususan kwa kuwa hakuna maneno “Ubadilishaji Mkubwa” au maneno mengine yanayohusiana kwenye maudhui. Jaribio la kuondoa maudhui kama hayo, ambayo hata yamezingatiwa kuwa marejeleo ya misimbo lingesababisha kuondolewa kwa kiasi kikubwa cha kauli zinazolindwa za kisiasa. Maudhui ambayo yamelindwa kimsingi hayapaswi “kuhusisisha na hatia” ama kwa sababu ya utambulisho wa mzungumzaji au kufanana kwa itikadi zenye chuki.
9. Uamuzi wa Bodi ya Usimamizi
Bodi ya Usimamizi inaunga mkono uamuzi wa Meta wa kuacha maudhui.
10. Mapendekezo
Uwazi
1. Meta inapaswa kutoa maelezo ya kina zaidi katika lugha ya Viwango vyake vya Jumuiya kuhsu Matamshi ya Chuki kuhusu jinsi inavyotofautisha majadiliano yanayohusiana na uhamiaji na matamshi ya chuki yenye madhara yanayolenga watu kulingana na hali yao ya uhamiaji. Hii inajumuisha kueleza jinsi kampuni hiyo inavyoshughulikia maudhui yanayoeneza nadharia za njama zenye chuki. Hii ni muhimu kwa watumiaji kuelewa jinsi Meta inavyolinda kauli za kisiasa kuhusu uhamiaji huku ikishughulikia madhara yanayoweza kutokea nje ya mtandao ya nadharia za njama zenye chuki.
Bodi itazingatia kuwa hili limetekelezwa wakati Meta itachapisha sasisho linaloeleza jinsi inavyoshughulikia majadiliano kuhusu uhamiaji katika muktadha wa Nadharia ya Ubadilishaji Mkubwa, na kuunganisha sasisho hilo kwa njia bayana katika Kituo cha Uwazi.
*Dokezo la Kiutaratibu:
Maamuzi ya Bodi ya Usimamizi yanatayarishwa na majopo ya Wanachama watano na kuidhinishwa na wanabodi wengi. Maamuzi ya Bodi hayawakilishi maoni ya kibinafsi ya Wanachama wote.
Kwa uamuzi wa kesi hii, utafiti huru ulipangwa kwa niaba ya Bodi. Bodi pia ilisaidiwa na Duco Advisors, shirika la ushauri linalolenga miingiliano ya siasa za ulimwengu, uaminifu na usalama na teknolojia. Memetica, shirika ambalo linajihusisha na utafiti wa chanzo huria kuhusu mienendo ya mitandao ya kijamii, pia ilitoa uchanganuzi. Utaalam wa lugha ulitolewa na Lionbridge Technologies, LLC, ambayo wataalamu wake wanajua lugha zaidi ya 350 na hufanya kazi kutoka miji 5,000 ulimwenguni kote.
العودة إلى قرارات الحالة والآراء الاستشارية المتعلقة بالسياسة