Decisión de casos múltiples
Utambulisho wa Jinsia na picha za uchi
17 de enero de 2023
Bodi ya Usimamizi imebatilisha maamuzi ya awali ya Meta ya kuondoa machapisho mawili ya Instagram yanayoonyesha watu waliobadilisha jinsia na watu wasio na jinsia yoyote wakiwa na vifua wazi.
2 casos incluidos en el paquete
IG-AZHWJWBW
Kesi kuhusu uombaji wa ngono kwenye Instagram
IG-PAVVDAFF
Kesi kuhusu uombaji wa ngono kwenye Instagram
Muhtasari wa kesi
Bodi ya Usimamizi imebatilisha maamuzi ya awali ya Meta ya kuondoa machapisho mawili ya Instagram yanayoonyesha watu waliobadilisha jinsia na watu wasio na jinsia yoyote wakiwa na vifua wazi. Pia inapendekeza kwamba Meta ibadilishe Kiwango chake cha Jumuiya kuhusu Picha za Uchi za Watu Wazima na Shughuli ya Ngono ili idhibitiwe na vigezo vilivyo wazi vinavyoheshimu viwango vya kimataifa vya haki za binadamu.
Kuhusu kesi hii
Katika uamuzi huu, Bodi ya Usimamizi inazingatia kesi mbili pamoja kwa mara ya kwanza. Sehemu mbili tofauti za maudhui yalichapishwa na akaunti moja ya Instagram, moja mnamo 2021, nyingine mnamo 2022. Akaunti hiyo hudumishwa na wanandoa wanaoishi Marekani ambao wanajitambulisha kama watu waliobadilisha jinsia na wasio wa jinsia yoyote.
Machapisho yote mawili yana picha za wanandoa hao na yanajumuisha vifua vyao vilivyo wazi huku chuchu zikiwa zimefunikwa. Manukuu ya picha hiyo yanajadili huduma ya afya ya watu waliobadilisha jinsia na yanasema kwamba mmoja wa wanandoa hivi karibuni atafanyiwa upasuaji wa hali ya juu (upasuaji wa kubadilisha jinsia ya kuunda kifua bapa), ambao wanandoa hao wanachangisha pesa ili kulipia.
Kufuatia mfululizo wa arifa za mifumo ya kiotomatiki ya Meta na ripoti kutoka kwa watumiaji, machapisho hayo yalikaguliwa mara nyingi kwa ukiukaji unaowezekana wa Viwango mbalimbali vya Jumuiya. Hatimaye Meta iliondoa machapisho yote mawili kwa kukiuka Viwango vya Jumuiya kuhusu Uombaji wa Ngono, inaonekana kwa sababu yana matiti na kiungo cha ukurasa wa kuchangisha pesa.
Watumiaji walikata rufaa kwa Meta na kisha kwa Bodi. Baada ya Bodi kukubali kesi hizo, Meta ilibaini kuwa imeondoa machapisho hayo kimakosa na kuyarejesha.
Matokeo muhimu
Bodi ya Usimamizi imegundua kuwa kuondoa machapisho haya hakulingani na Viwango vya Jumuiya ya Meta, maadili au wajibu wa haki za binadamu. Kesi hizi pia zinaangazia maswala ya kimsingi na sera za Meta.
Mwongozo wa ndani wa Meta kwa wasimamizi kuhusu wakati wa kuondoa maudhui chini ya sera ya Uombaji wa Ngono ni mpana zaidi kuliko mantiki iliyobainishwa ya sera hiyo, au mwongozo unaopatikana hadharani. Hili huleta mkanganyiko kwa watumiaji na wasimamizi na, kama vile Meta imetambua, husababisha maudhui kuondolewa kimakosa.
Katika angalau kesi moja, chapisho lilitumwa ili likaguliwe na binadamu na mfumo wa kiotomatiki uliofunzwa kutekeleza Kiwango cha Jumuiya kuhusu Picha za Uchi za Watu Wazima na Shughuli za Ngono. Kiwango hiki kinapiga marufuku picha zilizo na chuchu za kike isipokuwa katika hali maalum, kama vile kunyonyesha na upasuaji wa kuthibitisha jinsia.
Sera hii inatokana na mtazamo uwili wa kijinsia na tofauti kati ya miili ya kiume na ya kike. Mtazamo kama huo hufanya isieleweke wazi jinsi sheria zinavyotumika kwa watu wenye jinsia tofauti, wasiokuwa na jinsia yoyote na waliobadilisha jinsia, na inahitaji wakaguzi kufanya tathmini za haraka na zinazozingatia jinsia, ambayo haitumiki wakati wa kudhibiti maudhui kwa kiwango.
Vizuizi na vighairi kwa sheria za chuchu za kike ni vikubwa na vinatatanisha, haswa kwani vinatumika kwa watu waliobadilisha jinsia na watu wasiokuwa jinsia yoyote. Vighairi katika sera hii vinajumuisha maandamano, matukio ya kujifungua, na miktadha ya matibabu na afya, pamoja na upasuaji wa hali ya juu na uhamasishaji wa saratani ya matiti. Mara nyingi ni vigumu kuelewa vighairi hivi na hufafanuliwa vibaya. Katika baadhi ya miktadha, kwa mfano, lazima wasimamizi wakadirie kiwango na asili ya alama inayoonekana ili kubaini ikiwa vighairi fulani vitatumika. Ukosefu wa uwazi katika sera hii huzua hali ya kutokuwa na uhakika kwa watumiaji na wakaguzi, na kuifanya isiweze kutekelezeka kwa vitendo.
Bodi imesema mara kwa mara kwamba lazima Meta iwe makini na jinsi sera zake zinavyoathiri watu wanaopitia ubaguzi (tazama kwa mfano, maamuzi ya “Ukanda wa Wampum” na “Kurejesha maneno ya Kiarabu”). Hapa, Bodi inagundua kuwa sera za Meta kuhusu picha za uchi wa watu wazima husababisha vikwazo vikubwa zaidi kwa wanawake, watu wanaobadilisha jinsia na watu wasiokuwa na jinsia yoyote kujieleza kwenye mifumo yake. Kwa mfano, yana madhara makubwa katika muktadha ambapo kwa kawaida wanawake wanaweza kutembea wakiwa kifua wazi, na watu wanaojitambulisha kama LGBTQI+ wanaweza kuathirika kwa njia isiyo sawa, kama visa hivi vinavyoonyesha. Mifumo ya kiotomatiki ya Meta ilibainisha maudhui mara nyingi, licha ya kuwa hayakiuki sera za Meta.
Meta inapaswa kutafuta kuunda na kutekeleza sera ambazo zinashughulikia maswala haya yote. Inapaswa kubadilisha mbinu yake ya kudhibiti picha za uchi kwenye majukwaa yake kwa kufafanua vigezo vilivyo wazi vya kudhibiti sera ya Picha za Uchi za Watu Wazima na Shughuli za Ngono, ambayo inahakikisha watumiaji wote wanachukuliwa kwa njia inayolingana na viwango vya haki za binadamu. Inapaswa pia kuchunguza ikiwa sera ya Picha za Uchi za Watu Wazima na Shughuli ya Ngono inalinda dhidi ya kushiriki picha bila ridhaa, na kama sera zingine zinahitaji kuimarishwa katika suala hili.
Uamuzi wa Bodi ya Usimamizi
Bodi ya Usimamizi imebatilisha uamuzi wa awali wa Meta wa kuondoa machapisho hayo.
Bodi pia inapendekeza kwamba Meta:
- Ibainishe vigezo vilivyo wazi, vinavyolengwa na vinavyoheshimu haki ili kudhibiti Viwango vyake vya Jumuiya kuhusu Picha za Uchi za Watu Wazima na Shughuli za Ngono, ili watu wote wachukuliwe kwa njia inayolingana na viwango vya kimataifa vya haki za binadamu, bila kubaguliwa kwa misingi ya jinsia. Meta inapaswa kwanza kufanya tathmini ya kina ya athari za haki za binadamu kwa mabadiliko hayo, kushirikisha washikadau mbalimbali, na kuunda mpango wa kushughulikia madhara yoyote yaliyotambuliwa.
- Itoe maelezo zaidi katika Kiwango chake cha Jumuiya kuhusu Uombaji wa Ngono kinachotumika na umma kwa vigezo vinavyosababisha maudhui kuondolewa.
- Irekebishe mwongozo wake kwa wasimamizi wa Viwango vya Jumuiya kuhusu Uombaji wa Ngono ili kuonekana kwa usahihi zaidi sheria za umma kwenye sera. Hii inaweza kusaidia kupunguza makosa ya utekelezaji kwa upande wa Meta.
*Mihtasari ya kesi hutoa maelezo mafupi ya kesi na haina thamani ya kurejelewa katika kesi za baadaye.
Uamuzi kamili wa kesi
1. Muhtasari wa uamuzi
Bodi ya Usimamizi inabatilisha maamuzi ya kwanza ya Meta katika kesi mbili za machapisho ya Instagram yaliyoondolewa na Meta. Meta imekiri kuwa maamuzi yake ya kwanza katika kesi zote mbili yalikuwa na makosa. Kesi hizi zinaibua maswala muhimu kuhusu jinsi sera za Meta zinavyoathiri kwa njia isiyo sawa haki za watumiaji wanawake na wa jamii ya LGBTQI+ wa mifumo yake. Bodi inapendekeza kwamba Meta inapaswa kufafanua vigezo vilivyo wazi, vyenye lengo, vinavyoheshimu haki ili kudhibiti sera yake ya Picha za Uchi wa Watu Wazima na Shughuli za Ngono, kuhakikisha kuwa watu wote wanatendewa sawa kwa kuzingatia viwango vya kimataifa vya haki za binadamu, na kuepuka kubaguliwa kwa misingi ya jinsia au utambulisho wa kijinsia. Meta inapaswa kwanza kufanya tathmini ya kina ya athari za haki za binadamu ili kukagua athari za kupitishwa vigezo kama hivyo, ambavyo vinajumuisha ushirikishwaji wa washikadau kwa upana katika miktadha tofauti ya kiitikadi, kijiografia na kitamaduni. Kwa kiwango ambacho tathmini hii inapaswa kubainisha madhara yoyote yanayoweza kutokea, utekelezaji wa sera mpya unapaswa kujumuisha mpango wa kuyashughulikia.
Bodi inapendekeza pia kwamba Meta ifafanue sera yake ya Uombaji wa Ngono inayotumika na umma na kupunguza mwongozo wake wa utekelezaji wa ndani ili kulenga ukiukaji kama huo vizuri.
2. Maelezo ya kesi na historia
Kesi hizi zinahusu maamuzi mawili ya maudhui yaliyotolewa na Meta ambayo Bodi ya Usimamizi inashughulikia pamoja na uamuzi huu. Taswira mbili tofauti zenye manukuu zilichapishwa kwenye Instagram na akaunti moja ambayo inadumishwa kwa pamoja na wanandoa walio Marekani. Taswira zote mbili zinaangazia wanandoa, waliotaja kwenye machapisho yao, na kwenye mawasilisho yao kwa Bodi, kwamba wao wanajitambua kama wanaobadilisha jinsia na wasiokuwa na jinsia yoyote.
Meta iliondoa machapisho yote mawili chini ya Viwango vya Jumuiya kuhusu Uombaji wa Ngono. Katika kesi zote mbili, mifumo otomatiki ya Meta ilitambua maudhui hayo kama yenye uwezekano wa ukiukaji.
Katika picha ya kwanza, iliyotumwa mwaka wa 2021, watu wote wana kifua wazi na wana mkanda ulio na rangi ya nyama unaofunika chuchu zao. Katika taswira ya pili, iliyochapishwa 2022, mtu mmoja amevaa nguo huku mwenzake akiwa kifua wazi na wamefunika chuchu zao kwa mikono yao. Manukuu yanayoambatana na taswira hizi yanajadili jinsi mtu ambaye hajavaa nguo zozote kwenye picha zote mbili hivi karibuni atafanyiwa upasuaji wa hali ya juu wa kubadilisha jinsia ambayo itaunda kifua bapa. Wanaelezea mipango yao ya kutoa makala ya mchakato wa upasuaji huo na kujadili masuala ya huduma ya afya kwa watu wanaobadilisha jinsia. Wanatangaza kwamba wanachangisha fedha ili kulipia upasuaji huo kwa sababu wamekuwa na ugumu wa kupata bima ya upasuaji huo.
Katika kesi ya kwanza, picha hiyo iliainishwa kiotomatiki kuwa haiwezi kukiuka. Ripoti hiyo ilifungwa bila kukaguliwa na maudhui yalisalia kwenye jukwaa. Watumiaji watatu kisha waliripoti maudhui hayo kwa ponografia na kujidhuru. Ripoti hizi zilikaguliwa na waratibu binadamu ambao walipata kwamba chapisho hili si la ukiukaji. Maudhui yaliporipotiwa na mtumiaji kwa mara ya nne, mkaguzi mwingine binadamu aligundua kuwa chapisho hilo lilikiuka Kiwango cha Jumuiya kuhusu Uombaji wa Ngono na akaliondoa.
Katika kesi ya pili, chapisho hilo lilitambulishwa mara mbili na mifumo ya kiotomatiki ya Meta na kutumwa kwa ukaguzi wa binadamu ambapo lilikapatikana kuwa halikiuki. Watumiaji wawili kisha waliripoti maudhui hayo, lakini kila ripoti ilifungwa kiotomatiki bila kukaguliwa na binadamu na maudhui yalisalia kwenye Instagram. Hatimaye, mifumo ya kiotomatiki ya Meta ilitambua maudhui hayo kwa mara ya tatu na kisha kuyatumia kwa ukaguzi wa binadamu. Mara mbili zilizopita, kiainishaji cha kiotomatiki cha Picha za Watu Wazima na Shughuli ya Ngono kiliripoti maudhui hayo, lakini sababu ya ukaguzi huu unaorudiwa haijulikani wazi. Mkaguzi huyu binadamu wa mwisho alipata chapisho hili kuwa limekiuka Viwango vya Jumuiya kuhusu Uombaji wa Ngono na akaliondoa.
Wamiliki wa akaunti walikata rufaa dhidi ya maamuzi yote mawili ya uondoaji kwa Meta, na maudhui yalikaguliwa na wakaguzi binadamu katika kesi zote mbili. Hata hivyo, ukaguzi huu haukusababisha Meta kurejesha machapisho hayo. Wamiliki wa akaunti kisha walikata rufaa dhidi ya maamuzi ya kuondolewa kwa machapisho mawili kwa Bodi. Bodi inazingatia kesi hizi mbili kwa pamoja, jambo mpya kwa Bodi. Manufaa ya kufanya hivi ni kutambua masuala sawa katika sera na michakato ya maudhui ya Meta na kutoa masuluhisho ambayo yanashughulikia matatizo haya.
Baada ya Bodi kuchagua machapisho haya na Meta kuombwa itoe sababu za uamuzi wake wa kuondoa maudhui, Meta ilibaini uondoaji huo kuwa “makosa ya utekelezaji” na ikarejesha machapisho hayo.
Inapozingatia kwa nini kesi hizi zinawakilisha masuala muhimu, Bodi inabainisha kama muktadha unaofaa kiasi kikubwa cha maoni ya umma ambayo yalipokelewa katika kesi hizi, ambayo mengi yalikuwa kutoka kwa watu waliotambuliwa kama watu waliobadilisha jinsia, wasiokuwa na jinsia yoyote, au wanawake wenye jinsia ya kuzaliwa ambao walieleza kwamba waliathiriwa kibinafsi na makosa ya utekelezaji na masuala sawa na yale yaliyopo katika kesi hizi.
Bodi pia imebainisha kuwa muktadha unaofaa utafiti wa kitaaluma, pia ulionukuliwa katika maoni ya umma, na Haimson et al, Witt, Suzor na Huggins, na ripoti mbili za Salty kuhusu upendeleo wa algorithi na udhibiti wa jamii zilizotengwa. Tafiti hizi ziligundua kuwa makosa ya utekelezaji katika Viwango viwili vya Jumuiya vilivyojadiliwa katika kesi hizi yanaathiri wanawake na jumuiya ya LGBTQI+ kwa njia isiyo sawa. Mwandishi mwenza wa mojawapo ya tafiti hizi ni mwanachama wa Bodi ya Usimamizi.
3. Mamlaka na upeo wa Bodi ya Usimamizi
Bodi ina mamlaka ya kukagua uamuzi wa Meta kufuatia rufaa kutoka kwa mtumiaji ambaye maudhui yake yaliondolewa (Kifungu cha 2 cha Mkataba, Sehemu ya 1; Sheria ndogo za Kifungu cha 3, Sehemu ya 1).
Bodi inaweza kudumisha au kubatilisha uamuzi wa Meta (Kifungu cha 3, Sehemu ya 5 ya Mkataba), na kampuni itafuata uamuzi huu (Kifungu cha 4 cha Mkataba). Meta pia lazima itathmini uwezekano wa kutekeleza uamuzi wake kuhusiana na maudhui yanayofanana yaliyo katika muktadha tofauti (Kifungu cha 4 cha Mkataba). Maamuzi ya Bodi yanaweza kujumuisha taarifa za ushauri wa sera zenye mapendekezo ambayo Meta lazima iyajibu (Kifungu cha 3 cha Mkataba, Sehemu ya 4); Kifungu cha 4).
Bodi inapochagua kesi kama hii, ambapo Meta inakubali kwamba ilifanya makosa baada ya Bodi kubainisha kesi, Bodi hukagua uamuzi wa kwanza. Hii ni kuongeza ufahamu wa vigezo vya sera na michakato ya udhibiti wa maudhui ambayo yalisababisha makosa na kushughulikia masuala ambayo Bodi inabainisha na sera za kimsingi. Bodi pia inalenga kutoa mapendekezo ili kupunguza uwezekano wa makosa ya baadaye na kuwatendea watumiaji kwa haki zaidi kusonga mbele.
Bodi inapotambua kesi zinazoibua masuala yanayofanana, kesi hizo zinaweza kukabidhiwa jopo kwa wakati mmoja ili kujadiliwa kwa pamoja. Uamuzi wa kushurutisha utafanywa kuhusiana na kila kipande cha maudhui.
4. Vyanzo vya mamlaka
Bodi ya Usimamizi ilizingatia mamlaka na viwango vifuatavyo:
I. Maamuzi ya Bodi ya Usimamizi:
- Uamuzi wa “Kurejesha maneno ya Kiarabu” ( 2022-003-IG-UA). Bodi ilichanganua changamoto za kutumia vighairi vya sera na athari zisizolingana za baadhi ya chaguo za sera.
- Uamuzi wa “Mkanda wa Wampum” ( 2021-012-FB-UA). Bodi ilichanganua changamoto za kutumia vighairi vya sera na athari zisizolingana za baadhi ya chaguo za sera.
- “Dalili za saratani ya matiti na picha ya uchi” ( 2020-004-IG-UA). Bodi ilichanganua Miongozo ya Jumuiya ya Instagram na kupendekeza kwamba Meta ifafanue kuwa kuna kighairi cha ufahamu wa saratani ya matiti.
II. Sera za maudhui za Meta:
Kesi hizi zinahusisha Miongozo ya Jumuiya ya Instagram na Viwango vya Jamii ya Facebook. Kituo cha Uwazi cha Meta kinasema kwamba “Facebook na Instagram zinatumia sera sawa za Maudhui. Hii inamaanisha kwamba ikiwa maudhui yanazingatiwa kuwa ya ukiukaji kwenye Facebook, pia yanazingatiwa kuwa ya ukiukaji kwenye Instagram.”
Ushawishi wa Kingono
Miongozo ya Jumuiya ya Instagram inasema kuwa hairuhusiwi “kutoa huduma za ngono”. Sheria hii basi inaunganishwa na Kiwango cha Jumuiya ya Facebook kuhusu Uombaji wa Ngono.
Katika mtazamo wa sera kuhusu Uombaji wa Ngono, Meta inasema: “Tunaweka mpaka, hata hivyo, maudhui yakiwezesha, kuhimiza au kuratibu matukio ya ngono au huduma za kuuza ngono kati ya watu wazima. Tunafanya hivyo ili kuzuia uwezeshaji wa miamala inayoweza kujumuisha ulanguzi, kutumia nguvu na vitendo vya ngono bila idhini. Pia tunawekea mipaka lugha dhahiri ya kingono ambayo inaweza kusababisha uombaji wa ngono kwa sababu baadhi ya hadhira ndani ya jumuiya yetu kote ulimwenguni wanaweza kuathirika sana na aina hii ya maudhui na inaweza kuzuia uwezo wa watu kuunganishwa na marafiki zao na jumuiya pana zaidi.”
Kiwango cha Jumuiya ya Facebook kuhusu Uombaji wa Ngono kinasema kuwa Meta inapiga marufuku uombaji kwa njia iliyo wazi na isiyo wazi. Uombaji wa siri una vigezo viwili, ambavyo vyote ni lazima vitimizwe ili maudhui yakiuke sera. Ya kwanza ni “kutoa au kuomba” ambayo ni “Maudhui ambayo yanatoa au kuuliza moja kwa moja au kwa kukisia (kikawaida kupitia kutoa mbinu ya mwasiliani) kutoa au uombaji ngono.” Kigezo cha pili ni “vipengee vinavyopendekeza” ambavyo ni Maudhui ambayo yanatoa au kuuliza mambo yaliyotajwa hapa juu kwa kutumia vipengele vifuatavyo vinavyopendekeza kingono.” Vipengele vilivyoorodheshwa vinajumuisha “lugha ya msemo wa ngono” na “mikao.”
Picha za Uchi za Watu Wazima na Shughuli ya Ngono
Miongozo ya Jumuiya ya Instagram inasema kwamba watumiaji wanapaswa: “Kuchapisha picha na video ambazo zinafaa kwa ajili ya hadhira anuwai. Tunafahamu kwamba kuna nyakati ambazo watu wanaweza kutaka kushiriki picha za uchi ambazo ni kazi za kisanaa au ubunifu, lakini kwa sababu mbalimbali, haturuhusu picha za uchi kwenye Instagram. Hii ni pamoja na picha, video na baadhi ya maudhui yaliyoundwa kidijitali yanayoonyesha tendo la ngono, sehemu za siri na picha za karibu za makalio yaliyo uchi kikamilifu. Inajumuisha pia baadhi ya picha za chuchu za mwanamke katika muktadha wa kunyonyesha, nyakati za kujifungua na baada ya kujifungua, hali zinazohusiana na afya (kwa mfano, baada ya upasuaji wa kuondoa matiti, uhamasisho wa saratani ya matiti au upasuaji wa uthibitisho wa jinsia) au kitendo cha maandamano yanaruhusiwa.” Sehemu hii inaunganisha kwenye sera ya Facebook ya Picha za Uchi za Watu Wazima na Shughuli za Ngono ambayo inatoa maelezo zaidi kuhusu sheria hizi.
Kama sehemu ya mtazamo wa sera ya Kiwango cha Jumuiya kuhusu Picha za Uchi za Watu Wazima na Shughuli ya Ngono, Meta inaeleza kuwa: “Tunapiga marufuku kuonyeshwa kwa picha za uchi na shughuli za kingono kwa sababu baadhi ya watu ndani ya jumuiya yetu yote wanaweza kuathirika na aina hii ya maudhui. Kwa kuongezea, tunaondoa picha za ngono kwa chaguo-msingi ili kuzuia kushiriki kwa maudhui yasiyo kubalika au umri mdogo.”
Sera ya Facebook kuhusu Picha za Uchi za Watu Wazima na Shughuli za ngono pia inasema: “Usichapishe: Chuchu za mwanamke ambazo hazijafunikwa katika muktadha wa kunyonyesha, kujifungua na matukio ya baada ya kujifungua, muktadha wa kimatibabu au afya (kwa mfano, baada ya upasuaji wa kuondoa matiti, uhamasishaji wa saratani ya matiti, au upasuaji wa uthibitishio wa jinsia), au kitendo cha maandamano.” Watumiaji wanaweza pia kuchapisha picha za sehemu za siri zinaposhirikiwa katika “muktadha wa kimatibabu au kiafya” (ambayo inajumuisha upasuaji wa kuthibitisha jinsia) lakini lebo itatumiwa kuwaonya watu kuwa maudhui ni nyeti. Pia kuna angalau vipengele 18 vya ziada vya mwongozo wa ndani kuhusu chuchu na hali hizi zisizofuata kanuni.
III. Maadili ya Meta:
Maadili ya Meta yameorodheshwa katika utangulizi wa Viwango vya Jumuiya ya Facebook ambapo thamani ya “Sauti” inaelezewa kama “kikubwa”:
Kila mara, lengo la Viwango vyetu vya Jumuiya limekuwa ni kutengeneza mahali pa kujieleza na kuwapa watu sauti. […] Tunataka watu waweze kuzungumza kwa uwazi kuhusu masuala yaliyo muhimu zaidi kwao, hata kama baadhi ya watu wanaweza kutokubaliana nayo au kuona kuwa ni ya kupingwa.
Meta imeweka kikomo cha "Sauti" katika kuhudumia maadili manne, mawili kati ya hayo manne, ni muhimu hapa:
"Usalama": Tumejitolea kufanya Facebook kuwa mahali salama. Kujieleza kwa kutishia watu kuna uwezo wa kudhoofisha, kutenga au kunyamazisha wengine na hakukubaliki kwenye Facebook.
"Hadhi": Tunaamini kwamba watu wote wako sawa kihadhi na kihaki. Tunatarajia kwamba watu wataheshimu hadhi ya wenzao na hawatadhulumu au kuwashusha hadhi.
IV. Viwango vya kimataifa vya haki za binadamu:
Kanuni za Mwongozo wa Umoja wa Mataifa juu ya Biashara na Haki za Binadamu (UNGP), zilizoidhinishwa na Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa mnamo 2011, zina mfumo wa hiari wa majukumu ya haki za binadamu ya biashara za kibinafsi. Mnamo 2021, Meta ilitangazaSera yake ya Haki za Binadamu za Shirika, ambapo ilisisitiza tena kujitolea kwake katika kuwakilisha haki za kibinadamu kwa mujibu wa UNGP. Kigezo ambacho Bodi ilitumia katika kuchambua wajibu wa Meta kwa haki za binadamu katika kesi hizi kilitokana na viwango vifuatavyo vya haki za binadamu:
- Haki za uhuru wa kuwa na maoni na kujieleza: Kifungu cha 19, Mkataba wa Kimataifa kuhusu Haki za Raia na Kisiasa (ICCPR), Maoni ya Jumla Nambari 34, Kamati ya Haki za Kibinadamu, 2011; Mawasiliano 488/1992; Azimio 32/2, Baraza la Haki za Binadamu, 2016; Mjumbe Maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu uhuru wa maoni na kujieleza, anaripoti: A/HRC/38/35 (2018) na A/74/486 (2019).
- Haki za wanawake: Kifungu cha 2 na Kifungu cha 5, Mkutano kuhusu Kuondoa Aina zote za Ubaguzi dhidi ya Wanawake (CEDAW);
- Haki ya kutobaguliwa:: Article 2, aya ya 1 na Makala ya 26, ICCPR. Nepomnyashchiy dhidi ya Urusi, Kamati ya Haki za Binadamu, 2018 ( CCPR/C/123/D/2318/2013).
5. Mawasilisho ya mtumiaji
Katika mawasilisho yao ya kesi hizi, watumiaji wanasema kuwa wanaamini kuwa maudhui haya yaliondolewa kwa sababu ya kutopenda watu waliobadilisha jinsia. Wanaandika kwamba ikiwa Bodi ingethibitisha kwamba maudhui haya yanapaswa kubaki kwenye jukwaa, kwamba uamuzi huo ungechangia kufanya Instagram kuwa nafasi ya ukarimu zaidi kwa watu wa LGBTQI+ kujieleza.
6. Mawasilisho ya Meta
Meta ilieleza katika mantiki yake ya uamuzi kwamba uondoaji wa maudhui yote mawili ulikuwa makosa ya utekelezaji na kwamba hakuna chapisho lililokiuka sera zake za Uombaji wa Ngono. Meta inasema: “ofa au ombi pekee ni michango ya kuchangisha fedha au kutembelea tovuti ili kununua mashati, ambazo hazihusiani na uombaji wa ngono.”
Meta pia inasema kuwa hakuna chapisho linalokiuka Kiwango cha Picha za Uchi za Watu Wazima na Shughuli za Ngono. Mantiki hiyo inasema kwamba “mwongozo wa mkaguzi” wa ndani unashughulikia mahususi jinsi ya kuchukua hatua dhidi ya uchi wa watu wasio na jinsia yoyote, wasiopendelea jinsia yoyote, au waliobadilisha jinsia. Maudhui katika hali hizi yalishirikiwa katika “muktadha wazi wa wasiokuwa na jinsia yoyote au waliobadilisha jinsia kama inavyothibitishwa na mada ya jumla ya maudhui (kufanyiwa upasuaji wa hali ya juu) na lebo za reli zilizotumiwa.” Meta ilihitimisha kuwa "hata kama chuchu katika kesi hii zilionekana na zilikuwa wazi, hazingeweza kukiuka sera yetu ya Picha za Uchi wa Watu Wazima na Shughuli ya Ngono.” Meta pia ilikubali kuwa katika picha zote mbili, chuchu “zimefunikwa kabisa.”
Kwa kuzingatia muda uliopita tangu maudhui kuondolewa, Meta haikuweza kueleza Bodi sera ya mifumo yote ya kiotomatiki iliyobainisha maudhui kuwa yanayoweza kukiuka ambayo iliratibiwa kutekeleza Katika kesi moja, Meta iliweza kueleza kuwa maudhui yaliwekwa kwenye foleni ili yakaguliwe mara mbili na viainishaji vya Picha za Uchi za Watu Wazima na Shughuli za Ngono. Meta pia haikuweza kutoa maelezo yoyote kuhusu kwa nini wakaguzi walidhani kuwa maudhui yalikiuka sera ya Uombaji wa Ngono. Mantiki inakubali kwamba Meta “inafahamu kuwa baadhi ya wakaguzi wa maudhui wanaweza kuondoa kimakosa maudhui kama uombaji wa siri wa ngono (ingawa sivyo) kulingana na matumizi ya kiufundi kupita kiasi ya mwongozo wetu wa mkaguzi wa ndani.”
Bodi iliuliza Meta maswali 18, na Meta ikajibu yote.
7. Maoni ya umma
Bodi ya Usimamizi ilizingatia maoni 130 ya umma yanayohusiana na kesi hizi. Maoni tisini na saba kati ya hayo yaliwasilishwa kutoka Marekani na Kanada, 19 kutoka Ulaya, 10 kutoka Asia Pasifiki na Oshenia, moja kutoka Amerika ya Latini na Karibea, moja kutoka Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini, moja kutoka Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara na moja kutoka Asia ya Kati na Kusini.
Mawasilisho hayo yalihusu mada zifuatazo: uondoaji wa kimakosa wa maudhui kutoka kwa watumiaji waliobadilisha jinsia, wasiokuwa na jinsia yoyote, na wanawake; ukosefu wa haki na usawa wa tofauti za kijinsia ili kubaini aina za picha za uchi zinazoruhusiwa kwenye jukwaa; mkanganyiko kuhusu maudhui ambayo yanaruhusiwa chini ya Viwango vya Jumuiya kuhusu Picha za Uchi za Watu Wazima na Shughuli za Ngono, na Uombaji wa Ngono; na umuhimu wa mitandao ya kijamii kwa kujieleza katika jamii ambako haki za LGBTQI+ zinatishiwa.
Ili kusoma maoni ya umma yaliyowasilishwa kuhusu kesi hii, tafadhali bofya hapa. Maoni kadhaa yaliyowasilishwa hayajajumuishwa kwa vile yalikuwa na maelezo ya kibinafsi yanayowatambulisha watu wengine isipokuwa mtoa maoni.
8. Uchambuzi wa Bodi ya Usimamizi
Bodi iliangalia swali la iwapo machapisho haya yanapaswa kurejeshwa kwa Facebook kupitia lenzi tatu: Sera za maudhui ya Meta, maadili ya kampuni na majukumu yake ya haki za kibinadamu.
Bodi ilichagua kesi hizi kwa kuwa maudhui yasiyokiuka yaliyochapishwa na watu wanaojihusisha na makundi yaliyotengwa kunaathiri uhuru wao wa kujieleza. Hili ni muhimu sana kwani Instagram inaweza kuwa jukwaa muhimu kwa vikundi hivi kuunda jumuiya. Kesi hizi zinaonyesha jinsi makosa ya utekelezaji yanavyoweza kuwa na athari zisizo sawa kwa vikundi fulani na vinaweza kuashiria masuala makubwa zaidi katika sera na utekelezaji ambayo yanapaswa kurekebishwa.
8.1 Utiifu wa sera za maudhui za Meta
Bodi imegundua kuwa machapisho haya hayakiuki sera yoyote ya maudhui ya Meta. Ingawa Miongozo ya Jumuiya inatumika kwa Instagram, Meta pia inasema kuwa “Facebook na Instagram zinashiriki sera za maudhui. Maudhui ambayo yanazingatiwa kuwa ya ukiukaji kwenye Facebook pia yanazingatiwa kuwa ya ukiukaji kwenye Instagram.” Viwango vya Jumuiya ya Facebook vinatoa maelezo zaidi na vimeunganishwa kwenye Miongozo.
a. Uombaji wa Ngono
Kiwango cha Jumuiya kuhusu Uombaji wa Ngono kinasema kwamba uombaji wa ngono unahusisha mambo mawili:
- Maudhui ambayo yana ofa au ombi lisilo wazi NA
- Vipengee vinavyochochea ngono.
Ofa au ombi lisilo wazi.
Ofa au ombi lisilo wazi linafafanuliwa katika Kiwango cha Jumuiya kuhusu Uombaji wa Ngono kama “Maudhui ambayo yanatoa au kuuliza moja kwa moja au kwa kukisia (kikawaida kupitia kutoa mbinu ya mwasiliani) kutoa au uombaji ngono.” Katika “Maswali Yanayojulikana” ya Meta, ambayo hutoa mwongozo wa ziada wa ndani kwa wakaguzi, orodha ya maelezo ya mawasiliano ambayo husababisha uondoaji kama ofa isiyo wazi inajumuisha viungo vya wasifu wa mitandao ya kijamii na “viungo vya tovuti zinazotegemea usajili (kwa mfano, OnlyFans.com au Patreon. com).” Katika kesi hizi, maudhui yalitoa kiungo kwa jukwaa ambapo watumiaji walikuwa wakiandaa uchangishaji wa pesa ili kulipia upasuaji. Kwa sababu vigezo vya ndani vya Meta vinavyofafanua “ofa au ombi lisilo wazi” ni pana sana, kiungo hiki kitastahiki kitaalamu kuwa “toleo au ombi” chini ya mwongozo wa mkaguzi wa Meta licha ya kuwa hakikiuki kiwango kinachoonekana kwa umma, ambacho kinaonyesha kuwa ofa au ombi lazima liwe kwa ajili ya ngono.
Kipengele kinachochochea ngono.
Kiwango cha Jumuiya kinatoa orodha ya vipengele vinavyochochea ngono ambavyo vinajumuisha mikao. Maswali Yanayojulikana hutoa orodha, iliyofafanuliwa na Meta kama kamilifu, ya kile kinachojulikana kama mikao inayochochea ngono, ikijumuisha picha za uchi za “matiti ya kike yaliyofunikwa kidijitali au na sehemu za mwili wa binadamu au vitu.” Katika picha zote mbili, Bodi inabainisha kuwa kuna matiti yaliyofunikwa na sehemu za mwili wa binadamu (mikono) au vitu (utepe). Katika kesi hizi, maudhui kwenye machapisho yanaweka wazi kuwa wahusika wa picha wanatambulika kama watu waliobadilisha jinsia na wasiokuwa na jinsia yoyote, kumaanisha kuwa matiti yanayoonyeshwa ni ya watu ambao hawatambuliki kuwa wanawake. Bodi pia imegundua kuwa maudhui hayachochei ngono. Kwa msingi huo, kipengele cha pili kinachohitajika kukiuka sera ya Uombaji wa Ngono - kipengele kinachochochea ngono kama vile mkao wa kingono (ambao unajumuisha matiti ya kike yaliyofunikwa) - hakikutimizwa.
Kwa sababu kipengele cha pili hakikutimizwa, machapisho hayo hayakukiuka kiwango hiki. Kutumia toleo la umma la kipengele cha kwanza (ambacho kinaonyesha ni lazima ofa/ombi liwe kwa ajili ya kitu kinachohusiana na ngono) pia huonyesha kuwa picha hizi hazitajumuisha uombaji wa ngono.
b. Picha za Uchi za Watu Wazima na Shughuli ya Ngono
Kiwango cha Jumuiya kuhusu Picha za Uchi za Watu Wazima na Shughuli na Ngono kinasema kwamba watumiaji hawapaswi kuchapisha picha za “chuchu za mwanamke ambazo hazijafunikwa katika muktadha wa kunyonyesha, kujifungua na matukio ya baada ya kujifungua, muktadha wa kimatibabu au afya (kwa mfano, baada ya upasuaji wa kuondoa matiti, uhamasishaji wa saratani ya matiti, au upasuaji wa uthibitishio wa jinsia), au kitendo cha maandamano.” Maswali Yanayojulikana ya Meta yanasema zaidi kwamba wakaguzi wanapaswa kuruhusu “picha za chuchu zinaposhirikiwa katika muktadha wa mwanamke hadi mwanamume aliyebadilisha jinsia, asiyekuwa na jinsia yoyote, au asiyependendelea jinsia yoyote (k.m., mtumiaji anaonyesha utambulisho kama huo wa jinsia), bila kujali ukubwa au umbo ya matiti.” Hakuna picha yoyote katika kesi hizi inayokiuka Kiwango hiki cha Jumuiya.
Kwanza, hakuna kati ya picha hizo zinazoonyesha chuchu ambazo hazijafunikwa. Katika picha zote mbili, watu wamefunika chuchu zao kwa mikono au utepe. Pili, iwapo chuchu zingekuwa wazi, Bodi inabaini kwamba picha hizo zilishirikiwa na maandishi yanayoambatana ambayo yaliweka wazi kwamba watu hao wanatambuliwa kama wasiopendelea jinsia yoyote. Kwa hivyo sera hii haijakiukwa.
8.2 Utiifu wa maadili ya Meta
Bodi ilipata kwamba maamuzi yake ya kwanza ya kuondoa machapisho haya hayakuambatana na maadili ya Meta ya “Sauti” na “Hadhi” na hayakuhudumia maadili ya “Usalama.”
Makosa ya utekelezaji ambayo huathiri kwa njia isiyo sawa vikundi vinavyokabiliwa na ubaguzi huleta tishio kubwa kwa “Sauti” na “Heshima.” Ingawa hoja za haki za binadamu za Meta zilijadili “Usalama,” hasa zinazohusiana na kushiriki picha bila ridhaa, biashara haramu ya ngono na unyanyasaji wa watoto, Bodi inagundua kwamba uondoaji huu haukuendeleza “Usalama.”
8.3 Utiifu wa wajibu wa haki za binadamu wa Meta
Uhuru wa kujieleza (Kifungu cha 19 ICCPR)
Kifungu cha 19 cha ICCPR kinatoa ulinzi mpana wa kujieleza, ikijumuisha majadiliano ya haki za binadamu na kujieleza ambayo watu wanaweza kuchukulia kuwa “ya kuudhi sana” (Maoni ya Jumla 34, aya ya 11). Haki ya uhuru wa kujieleza inahakikishwa kwa watu wote bila ubaguzi kuhusu “ngono” au “hadhi nyingine” ( ICCPR, Kifungu cha 2, aya ya 1). Kamati ya Haki za Kibinadamu imethibitisha katika kesi kama vile Nepomnyashchiy v Urusi ( CCPR/C/123/D/2318/2013) kwamba kizuizi cha ubaguzi kinajumuisha ubaguzi kwa misingi ya utambulisho wa kijinsia.
Maudhui hayo yanahusiana na masuala muhimu ya kijamii. Kwa watumiaji hawa, Instagram hutoa jukwaa la kujadili na kuwakilisha usemi wao wa kijinsia, ikitoa jukwaa la kufanya miunganisho na kupata usaidizi. Maudhui hayo yanaweza pia kuathiri moja kwa moja uwezo wa watumiaji kutekeleza upasuaji wa kuthibitisha jinsia, kwa kuwa machapisho yote mawili yanaeleza kuwa mtu mmoja atafanyiwa upasuaji wa hali ya juu na atashiriki uchangishaji ili kulipia gharama za upasuaji huo.
Kifungu cha 19 kinahitaji kwamba pale ambapo serikali imeweka vikwazo dhidi ya semi, vikwazo hivyo lazima vitimize masharti ya kutii sheria, lengo halali na umuhimu na ulinganifu ( ICCPR, Kifungu cha 19, aya ya 3). Kwa kutegemea utaratibu wa UNGP, Mjumbe Maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu uhuru wa mawazo na kujieleza ametoa mwito kwa kampuni za mitandao ya kijamii kuhakikisha kwamba kanuni zao za maudhui zinaongozwa na masharti ya Kipengele cha 19, aya ya 3, ICCPR ( A/HRC/38/35, aya ya 45 na 70). Bodi imetumia mfumo huu wa kuchanganua sera za na utekelezaji wa Meta.
Katika kesi hii, Bodi inagundua kuwa Meta haijatimiza wajibu wake wa kuunda na kutekeleza sera zinazolingana na viwango hivi. Vigezo vya ndani vinavyotumika kuondoa maudhui chini ya sera ya Uombaji wa Ngono ni kubwa zaidi kuliko mantiki iliyobainishwa ya sera hiyo, pamoja na athari za utekelezaji kupita kiasi ambazo Meta yenyewe imetambua. Kiwango cha Jumuiya kuhusu Picha za Uchi za Watu Wazima na Shughuli za Ngono huathiri kwa njia isiyo sawa wanawake na watumiaji wa LGBTQI+ na hutegemea mitazamo ya dhamira na ya kukisia kuhusu jinsia ambayo haiwezi kutekelezeka wakati wa kujihusisha katika udhibiti wa maudhui kwa kiwango. Bodi huchanganua mapungufu haya na kupendekeza Meta ianze mchakato mpana wa kushughulikia matatizo haya.
I. Kutii sheria (uwazi na upatikanaji wa sheria)
Lazima sheria zinazozuia usemi ziwe wazi na ziweze kufikiwa ili wote wanaowajibika kuzitekeleza, na watumiaji, wajue kinachoruhusiwa. Viwango vyote vya Jumuiya vinavyozingatiwa katika kesi hizi havifikii kiwango hicho.
a. Uombaji wa Ngono
Bodi imegundua kuwa Kiwango cha Jumuiya kuhusu Uombaji wa Ngono kina vigezo vya ziada katika miongozo ya ndani inayotolewa kwa wakaguzi. Mwongozo huu ambao haukuundwa vizuri huchangia kwa utekelezaji zaidi wa wakaguzi na watumiaji kuchanganyikiwa. Meta ilikubali jambo hili, kwani ilieleza Bodi kwamba kutumia mwongozo wake wa ndani kunaweza “kusababisha utekelezaji kupita kiasi” katika kesi ambapo vigezo vya uombaji usio wazi wa ngono vinatimizwa lakini ni wazi kwamba “hakukuwa na nia ya kuomba ngono.”
Mkanganyiko huo unaonyeshwa katika vipengele vyote viwili vya sera hii. Kuhusiana na kipengele cha ‘ofa na ombi’ cha Kiwango cha Jumuiya kuhusu Uombaji wa Ngono, kanuni zinazotumika na umma hurejelea “njia ya kuwasiliana” kwa mhusika anayeomba. Hata hivyo, mwongozo wa wasimamizi, Maswali Yanayojulikana, unasema kwamba “njia ya mawasiliano” kwa ajili ya 'ofa au ombi' isiyo wazi inajumuisha viungo vya wasifu wa mitandao ya kijamii au viungo vya tovuti za wahusika wengine kulingana na usajili kama vile Patreon. Haijafafanuliwa wazi kwa watumiaji kuwa kiungo chochote cha wasifu mwingine wa mitandao ya kijamii, jukwaa la malipo la wahusika wengine au kiungo cha kuchangisha pesa (kama vile Patreon au GoFundMe) kinaweza kumaanisha kuwa chapisho lao linachukuliwa kama ombi. Mkanganyiko huu unaonyeshwa katika maoni mengi ya umma ambayo Bodi ilipokea kutoka kwa watu ambao hawakuelewa kwa nini maudhui pamoja na viungo vya wahusika wengine yaliondolewa au kusababisha akaunti zao kupigwa marufuku.
Kigezo cha pili, kinachohitaji kipengele kinachochochea ngono, ni pana na sio dhahiri, na pia hakilingani na sera ya Meta ya Picha za Watu Wazima na Shughuli za Ngono. Kiwango cha Jumuiya kinachotumika na umma kinajumuisha “mikao inayochochea ngono” kama kipengele cha kuchochea ngono. Maswali Yanayojulikana kisha yanatoa orodha ya kina ya “mikao ya kuchochea ngono” ambayo inajumuisha kuwa kifua wazi na kufunika matiti kwa mikono au vitu. Huenda watumiaji wasiweze kutabiri kuwa picha yoyote yenye matiti iliyofunikwa inachukuliwa kuwa mkao unaochochea ngono. Mkanganyiko huu unachangiwa na ukweli kwamba sera ya Picha za Uchi za Watu Wazima inaruhusu picha za kifua wazi ambapo chuchu zimefunikwa. Kwa hali hii, maudhui ambayo yanachukuliwa kuwa ya ngono chini ya sera moja hayazingatiwi kuwa ya ngono chini ya sera nyingine.
Mbali na mtumiaji kutokuwa na uhakika, ukweli kwamba wakaguzi walipata matokeo tofauti mara kwa mara kuhusu maudhui haya inaonyesha ukosefu wa uwazi kwa wasimamizi kuhusu maudhui ambayo yanafaa kuzingatiwa kuwa ya uombaji wa ngono.
Kama vile Meta inavyokubali, matumizi ya mwongozo wake wa ndani kuhusu vipengele viwili vya maombi ya siri ni kuondoa maudhui ambayo hayatafuti vitendo vya ngono. Kwa muda mrefu, uondoaji wa kimakosa unaweza kushughulikiwa vyema kwa kurekebisha upeo wa sera hii. Hata hivyo, katika kipindi mfupi, Bodi inapendekeza kwamba Meta irekebishe miongozo yake ya ndani ili kuhakikisha kuwa vigezo vinaangazia kanuni zinazotumika na umma na kuhitaji muunganisho ulio wazi kati ya “ofa na ombi” na “kipengele cha kuchochea ngono.” Meta inapaswa pia kuwapa watumiaji maelezo zaidi kuhusu “ofa au ombi” la ngono na kinachojumuisha mikao ya kuchochea ngono katika Viwango vya Jamii vya umma.
b. Picha za Uchi za Watu Wazima na Shughuli ya Ngono
Kiwango cha Picha za Uchi za Watu Wazima na Shughuli za Ngono kinazingatia tofauti za kijinsia ambazo ni ngumu kutekeleza na kina vighairi ambavyo havijabainishwa vyema. Baadhi ya sheria katika sera zitawachanganya watumiaji, ambao hawajui kinachoruhusiwa. Hili pia husababisha mkanganyiko kwa wasimamizi, ambao lazima wafanye tathmini za kibinafsi kulingana na maelezo yasiyo kamili ambayo hayawezi kuepukika na kutumia sheria kwa haraka yenye vipengele, vizuizi, na dhana nyingi.
Licha ya kutumia lugha inayoangazia sehemu mahususi za mwili badala ya jinsia (na kuruhusu watumiaji kuchagua kutoka kwa aina mbalimbali za utambulisho wa kijinsia kwenye wasifu wao), sheria nyingi za Meta hazielezi jinsi kampuni inavyoshughulikia maudhui yanayoonyesha watu wa jinsia tofauti, waliobadilisha jinsia au wasiokuwa na jinsia yoyote. Kwa mfano, sera inarejelea “sehemu ya uzazi ya mwanamume na mwanamke,” “matiti ya kike” na “chuchu za kike,” lakini haijulikani jinsi maelezo haya yanavyotumika kwa watu walio na miili na vitambulisho ambavyo vinaweza kuwa havilingani na ufafanuz huu. Watu wengi waliobadilisha jinsia na wasiokuwa na jinsia yoyote waliwasilisha maoni ya umma kwa Bodi wakisema kuwa watumiaji hawajui ikiwa maudhui yao yanatathminiwa na kuainishwa kulingana na utambulisho wao wa kijinsia, jinsia waliyopewa walipozaliwa, au vipengele vya mwonekano wao wa kimwili.
Sheria za sasa zinahitaji wakaguzi binadamu kutathmini kwa haraka jinsia ya mtumiaji, kwani sera hii inatumika kwa “chuchu za kike,” na utambulisho wao wa kijinsia, kwa kuwa kuna vighairi kulingana na ikiwa mtu aliyeonyeshwa hana jinsia yoyote, hapendelei jinsia yoyote, aliyebadilisha jinsia, au kuchapisha katika muktadha wa upasuaji wa kuthibitisha jinsia. Mitazamo ya jinsia na ngono inahitaji tafsiri ya vidokezo vya muktadha na mwonekano, zote ambazo ni maamuzi ya kibinafsi yanasababisha makosa.
Mbinu hii inakanganya zaidi kwa “kanuni ya chaguo-msingi ya Meta kwa mwanamke” ambapo sera zenye vikwazo zaidi zinazoweza kutumika kwa uchi wa kike (kinyume na wanaume) hutumika katika hali za mashaka. Maswali Yanayojulikana yanasema kwamba pale ambapo hakuna muktadha unaoeleweka na mtu kwenye picha hiyo “anajiwasilisha kama muktadha wa mabadiliko ya jinsia ya mwanamke AU mwanamume kwa mwanamke, basi chaguo-msingi kwa uchi wa kike na kutumia sera husika.”
Idadi ya vizuizi na vighairi kwa kanuni za chuchu zinazochukuliwa kuwa za kike ni kubwa na ya kutatanisha. Vighairi vinajumuisha vitendo vya kupinga matukio ya kuzaa na kunyonyesha, hadi miktadha ya matibabu na afya, pamoja na picha za baada ya upasuaji wa kuondoa matiti na uhamasishaji kuhusu saratani ya matiti. Vighairi mara nyingi havifafanuliwa au vimefafanuliwa vibaya. Orodha ya vighairi pia imekua kwa kiasi kikubwa baada ya muda na inaweza kutarajiwa kuendelea kukua kadri usemi unavyoendelea. Inapohusu suala la matiti ya wanawake, sera ya Meta ya Picha za Uchi za Watu Wazima na Shughuli ya Ngono ya inafanya dhana chaguo-msingi kuwa vielelezo kama hivyo vinajumuisha picha ya ngono. Hata hivyo orodha inayopanuka ya vighairi huonyesha kwamba, chini ya hali nyingi zinazotambuliwa katika sera, picha za matiti ya wanawake hazichochei ngono.
Hata katika kila kighairi, maswali mengi hutokea. Kwa mfano, kighairi cha upasuaji wa uthibitishaji wa jinsia kina umuhimu mahususi kwa watumiaji waliobadilisha jinsia na wasiokuwa na jinsia yoyote, lakini Meta haitoi maelezo ya upeo wa kighairi chake cha upasuaji wa uthibitishaji wa jinsia katika sheria zake zinazotumika na umma. Hili limesababisha maoni mengi ya umma kutolewa ambayo yanaonyesha mkanganyiko kuhusu iwapo maudhui yanayoruhusiwa chini ya kighairi yanaweza kujumuisha picha za kabla ya upasuaji (ili kuunda picha ya kabla na baada) na picha za wanawake waliobadilisha jinsia ambao wamepokea nyongeza za matiti. Miongozo ya ndani na Maswali Yanayojulikana yanaweka wazi kwamba kighairi hiki ni ndogo kuliko jinsi mwongozo wa umma unavyoweza kufasiriwa kumaanisha.
Sera za Meta zinatokana na tofauti mbili kati ya mwanamume na mwanamke, na hivyo kuleta changamoto wakati Meta inajaribu kueleza kighairi chake cha upasuaji wa uthibitishaji wa jinsia. Katika majibu ya Meta kwa Bodi, Meta ilieleza kuwa kighairi cha upasuaji wa uthibitisho wa jinsia kinamaanisha kwamba inaruhusu “chuchu za kike ambazo hazijafunikwa kabla ya mtu kufanyiwa upasuaji wa juu ili kuondoa matiti yake, wakati maudhui yanashirikiwa katika muktadha wa mwanamke hadi mwanamume aliyebadilisha jinsia, asiyekuwa na jinsia yoyote, au asiyependendelea jinsia yoyote.” Kanuni hizo zaidi zinasema “Chuchu za wanawake waliobadilsha jinsia kutoka kwa mwanamume kwenda kwa mwanamke waliofanyiwa nyongeza ya matiti (upasuaji wa hali ya juu) haziruhusiwi, isipokuwa kama kuna alama kwenye chuchu inaonekana.”
Mwongozo wa ndani kuhusu alama za upasuaji na chuchu ni ngumu kueleweka zaidi. Sheria za upasuaji wa kuondoa matiti, kwa mfano, huruhusu “Matukio ambapo chuchu zinatengenezwa upya kutoka kwa tishu nyingine au kuchorwa” na “matukio ambapo angalau titi moja lililotolewa kwa upasuaji lipo, hata kama chuchu nyingine ya kike iliyo wazi inaonekana.” Jambo la kutatanisha zaidi, kanuni inasema kwamba “Kwa upasuaji wa kuondoa matiti, alama inajumuisha picha ya eneo ambalo tishu za matiti zilizoondolewa zilikuwa. Alama halisi ya upasuaji haihitaji kuonekana.”
Wakaguzi wanaweza kutatizika kutumia kanuni zinazohitaji kwamba watathmini kwa haraka sifa mahususi za jinsia za mtu aliyeonyeshwa ili kuamua kama watatumia sheria za chuchu za kike, na kisha jinsia ya mtu huyo ili kubaini ikiwa baadhi ya vighairi vitatumika, na kisha kuzingatia ikiwa maudhui hayo yanaonyesha mwanzo au matokeo ya upasuaji, utaratibu gani wa upasuaji, na ukubwa na asili ya alama inayoonekana, ili kubaini iwapo vighairi vingine vinaweza kutumika. Picha sawa ya chuchu zinazowasilisha wanawake haitapigwa marufuku ikiwa itachapishwa na mwanamke wenye jinsia ya kuzaliwa lakini itaruhusiwa ikiwa imechapishwa na mtu anayejitambulisha kama mtu asiyekuwa na jinsia yoyote. Bodi pia inabainisha vighairi vya ziada vinavyohusiana na chuchu kulingana na miktadha ya kupinga, kuzaa, baada ya kuzaliwa, na kunyonyesha ambayo haikuyachunguza hapa, lakini pia lazima yatathminiwe na yahusishe vigezo vya ndani vya ziada.
Kwa kuzingatia umuhimu wa haki za kujieleza kuhusu masuala ya jinsia, afya ya kimwili, kuzaa na uzazi, kazi ngumu ya sasa ya vighairi huzua hali ya watumiaji kutokuwa na uhakika na inaweza kuwa na sheria zilizotumika vibaya, kama inavyothibitishwa na kesi hii. Ukosefu wa uwazi kwa watumiaji na wasimamizi waliomo katika sera hii hufanya kiwango kisiweze kutelezeka. Kama ilivyojadiliwa zaidi hapa chini, Bodi inaamini kuwa Meta inapaswa kutumia mtazamo wa picha za uchi wa watu wazima ambao unahakikisha kuwa watu wote wanatendewa bila kubaguliwa kwa misingi ya jinsia au utambulisho wa kijinsia.
II. Lengo halali
Kifungu cha 19 cha ICCPR kinasema kwamba serikali zinapozuia kujieleza, zinaweza tu kufanya hivyo ili kuendeleza malengo halali, ambayo yameelezwa kama: “kuheshimu haki au sifa za wengine . . . [na] ulinzi wa usalama wa taifa au wa utaratibu wa umma (ordre public), au wa afya na maadili ya umma.” Uamuzi huu unachunguza sababu za Meta za kuzuia usemi katika sera zake kwa kuzingatia viwango hivi.
a. Uombaji wa Ngono
Meta inaeleza katika sera yake ya Uombaji wa Ngono kwamba "inakusudiwa kuzuia watumiaji kutumia Facebook au Instagram kuwezesha “shughuli ambazo zinaweza kuhusisha biashara haramu ya binadamu, kulazimishwa na vitendo vya ngono bila ridhaa” ambavyo vinaweza kutokea nje ya jukwaa. Huu ni mfano wa kulinda haki za wengine, jambo ambalo ni lengo halali.
b. Picha za Uchi za Watu Wazima na Shughuli ya Ngono
Meta ilitoa hoja kadhaa kwa vipengele mahususi vya sera yake ya Picha za Uchi za Watu Wazima na Shughuli za Ngono, pamoja na kuzuia usambazaji wa maudhui yasiyo ya ridhaa, kuwalinda watoto pale ambapo umri wa mtu hauko wazi na ukweli kwamba, “baadhi ya watu katika jumuiya yetu wanaweza kuathirika na aina hii ya maudhui.” Meta pia ilitoa ufafanuzi wa kanuni zake za jumla kuhusu picha za uchi kwa Bodi. Inasema kuwa “Katika kuandaa sera yetu, Meta ilizingatia (1) hali ya faragha au nyeti ya picha hiyo; (2) ikiwa idhini ilitolewa katika kuchukua na kushiriki picha za uchi; (3) hatari ya unyanyasaji wa kingono; na (4) ikiwa picha hizo kufichuliwa kunaweza kusababisha unyanyasaji nje ya jukwaa, hasa katika nchi ambazo picha hizo zinaweza kuchukiza kitamaduni.”
Malengo haya mengi yanalingana na kulinda haki za wengine. Hata hivyo, mantiki ya Meta ya kulinda “hisia ya jamii” inafaa uchunguzi zaidi. Mantiki hii ina uwezo wa kulinganisha na lengo halali la “maadili ya umma.” Licha ya hayo, Bodi inabainisha kuwa lengo la kulinda “maadili ya umma” wakati mwingine limekuwa likitumiwa isivyofaa na wadhibiti wa hotuba za serikali ili kukiuka haki za binadamu, hasa za wanachama wa wachache na makundi yaliyo hatarini. Kamati ya Haki za Kibinadamu imetahadharisha kwamba “dhana ya maadili inatokana na desturi nyingi za kijamii, kifalsafa na kidini; kwa hivyo, vikwazo... kwa madhumuni ya kulinda maadili lazima yajikite kwenye kanuni ambazo hazitokani pekee na utamaduni mmoja” (Kamati ya Haki za Kibinadamu, Maoni ya Jumla 34)
Ingawa sheria ya haki za binadamu inatambua kwamba maadili ya umma yanaweza kujumuisha lengo halali la vikwazo vya uhuru wa kujieleza kwa majimbo, na vikwazo vya picha za uchi hadharani vipo duniani kote, Meta inasisitiza malengo mengine isipokuwa “hisia za jamii” katika muktadha mahususi wa kesi hii. Meta alisema kuwa “ingawa sera [yake] ya picha za uchi inaambatana na ulinzi wa maadili ya umma [...] haitegemei lengo hili kwa sababu viwango vya maadili kuhusu picha za uchi vinatofautiana sana katika tamaduni zote na havitatekelezeka kwa kiwango.” Kwa mfano, katika jumuiya nyingi na sehemu nyingi za dunia, maonyesho ya watu waliobadilisha jinsia na wasiokuwa na jinsia yoyote walio matiti wazi yanaweza kuchukuliwa kuwa yanaathiri hisia ya jumuiya. Ingawa Meta haizuii usemi kama huo. Zaidi ya hayo, Bodi inajali kuhusu mzigo unaojulikana na unaorudiwa usio na uwiano wa usemi ambao umekabiliwa na wanawake, watu waliobadilisha jinsia, na watu wasiokuwa na jinsia yoyote kwa sababu ya sera za Meta (tazama hapa chini). Kwa sababu hizi, Bodi inazingatia malengo mengine zaidi ya “hisia za jumuiya” ambazo Meta imeendeleza katika kuchunguza wajibu wake wa haki za binadamu.
Tunapaswa kukumbuka kwamba baadhi ya sababu ambazo Meta hutoa kwa sera yake ya picha za uchi huakisi dhana asili ya kupendekeza ngono kwa matiti ya wanawake kama msingi. Bodi ilipokea maoni ya umma kutoka kwa watumiaji wengi ambao walionyesha wasiwasi kuhusu unyanyasaji wa kijinsia wa miili ya wanawake waliobadilisha jinsia na wasiokuwa na jinsia yoyote, wakati hakuna dhana inayoweza kulinganishwa ya kingono ambayo inatumika kwa wanaume wenye jinsia ya kuzaliwa. (Angalia, k.m., Maoni ya Umma 10624 iliyowasilishwa na InternetLab).
Bodi ilipokea maoni mengi ya umma katika kesi hii kupitia michakato yake ya kawaida ya kufikia watu. Kama shirika lililojitolea kutoa kiwango fulani cha uwajibikaji kwa watumiaji wa Meta na washikadau wakuu, Bodi inazingatia maoni kwa uzito kama sehemu ya mijadala yake. Kama ilivyo kwa kesi zote, tunaelewa kuwa huenda maoni haya huenda yasiwe yanawakilisha maoni ya kimataifa. Bodi inathamini uzoefu na utaalamu ulioshirikiwa kupitia maoni na inaendelea kuchukua hatua ili kuongeza upana wa ufikiaji wake kwa jumuiya ambazo huenda hazishiriki katika mchakato huu kwa sasa.
Hatimaye, Bodi inatambua kuwa Meta inaweza kuchangia kihalali katika umuhimu wa kuzuia madhara fulani ambayo yanaweza kuwa na athari kwa jinsia. Kama ilivyobainishwa na Mwandishi Maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu unyanyasaji dhidi ya wanawake, ni “muhimu kutambua kwamba intaneti inatumiwa katika mazingira mapana ya ubaguzi wa kimuundo na wa kimfumo ulioenea na unyanyasaji wa kijinsia dhidi ya wanawake na wasichana” (A/HRC/ 38/47). Zaidi ya hayo, tafiti zinaonyesha kuwa “asilimia 90 ya wale walioathiriwa na usambazaji usio na ridhaa wa kidijitali wa picha za siri ni wanawake.” (A/HRC/38/47). Meta inapaswa kutafuta kuzuia madhara ya kijinsia, katika utekelezaji kupita kiasi na utekelezaji mdogo wa uzuizi wa picha za uchi.
III. Umuhimu na uwiano
Bodi imegundua kuwa sera za Meta, kama zilivyoandaliwa na kutekelezwa, zinanasa maudhui zaidi kuliko inavyohitajika. Hakuna sera inayolingana na maswala ambayo wanajaribu kushughulikia.
a. Uombaji wa Ngono
Ufafanuzi wa sera ya Uombaji wa Ngono kuhusu “ofa au ombi” na mikao inayochochea ngono inapita kiasi na inafaa kunasa idadi kubwa ya maudhui ambayo hayahusiani na uombaji wa ngono. Meta yenyewe inakubali hatari ya utekelezaji mbaya, ikisema “inafahamu kuwa baadhi ya wakaguzi wa maudhui wanaweza kuondoa kimakosa maudhui kama uombaji wa siri wa ngono (ingawa sivyo) kulingana na matumizi ya kiufundi kupita kiasi ya mwongozo wake wa mkaguzi wa ndani.” Meta iliaendelea:
Kwa sasa, kulingana na Maswali Yetu Yanayojulikana, tunazingatia kushiriki, kutaja, au kutoa maelezo ya mawasiliano ya utambulisho wa kijamii au wa kidijitali kuwa ofa au ombi lisilo wazi la ngono. […] Hata hivyo, kutumia mwongozo huu kunaweza kusababisha utekelezaji kupita kiasi katika kesi ambapo, kwa mfano, mtu anachukuliwa na mkaguzi kuwa amejiweka kwa njia inayochochea ngono (inakidhi kigezo cha “kipengele cha kuchochea ngono”) na kumtambulisha mpiga picha ili kumpa sifa kwa ajili ya picha hiyo (inafikia kigezo cha “ofa au ombi”). Aina hii ya maudhui hayakiuki kwa sababu hakuna nia ya kuomba ngono, lakini bado yanaweza kuondolewa (kinyume na sera) kwa sababu yanakidhi vigezo viwili vilivyoainishwa hapo juu.
UNESCO, katika ripoti inayojadili elimu katika mazingira ya kidijitali, ilieleza hatari ya utekelezaji wa kimakosa kupita kiasi. Ikibainisha kuwa “Kanuni kali kuhusu kushiriki picha chafu kunamaanisha kwamba, wakati fulani, nyenzo za kielimu zilizochapishwa mtandaoni ili kusaidia kujifunza kuhusu mwili, au mahusiano ya kingono, zinaweza kudhaniwa kimakosa na wasimamizi kuwa maudhui yasiyofaa na yaliyo wazi kwa hivyo kuondolewa kwenye majukwaa ya kawaida ya wavuti. .” Bodi pia inabainisha maoni mengi ya umma ambayo ilipokea yaliyojadili uondoaji usiofaa chini ya Kiwango hiki. Kwa mfano, ACON, (NGO ya elimu ya HIV nchini Australia) inaandika kwamba maudhui ambayo yalitangaza ujumbe wa kuzuia HIV kwa njia chanya ya ngono na maudhui yanayotangaza warsha za elimu yameondolewa kwa ajili ya uombaji wa ngono. Hii imesababisha NGO kuchagua lugha katika maudhui yao ili kuepuka uondoaji wa Meta, badala ya kuchagua lugha bora zaidi ya kufikia jamii zinazolengwa (Maoni ya Umma 10550). Hili liliungwa mkono na Joanna Williams, mtafiti ambaye aligundua kwamba mashirika tisa kati ya kumi na mawili ya afya ya ngono aliyohoji yaliripoti kwamba yameathiriwa vibaya na usimamizi wa Meta katika eneo hili (Maoni ya Umma 10613).
b. Picha za Uchi za Watu Wazima na Shughuli ya Ngono
Mbali na changamoto katika kuweka sheria zinazoweza kutekelezeka na zinazoweza kuepukika kulingana na mtazamo wa Meta kuhusu ngono na utambulisho wa kijinsia, kama ilivyoelezwa hapa juu, Bodi pia imegundua kuwa sera za Meta kuhusu picha za uchi za watu wazima zinaweka vizuizi visivyolingana kwa baadhi ya aina za maudhui na usemi. Sera hizo zinaamuru uondoaji wa maudhui, wakati hatua zenye vikwazo kidogo zinaweza kufikia malengo ya sera yaliyotajwa.
Tayari Meta hutumia aina mbalimbali za utekelezaji kando na uondoaji, pamoja na kutumia skrini za maonyo na maudhui ya kuzuia umri ili kuruhusu watumiaji walio na umri wa zaidi ya miaka 18 pekee kuyatazama. Zaidi ya hayo, tayari inatumia hatua kama hizo ndani ya sera yake ya Picha za Uchi za Watu Wazima na Shughuli za Ngono, ikijumuisha kwa maonyesho ya kisanii ya shughuli za ngono. Meta pia inaweza kutaka kushirikisha wasimamizi wa kiotomatiki na binadamu ili kufanya uboreshaji zaidi, uamuzi mahususi wa muktadha wakati muktadha wa uchi ni wa ngono, bila kujali jinsia ya mwili inayoonyeshwa. Meta inaweza kutumia zaidi hatua mbalimbali za sera ili kudhibiti mwonekano wa maudhui picha za uchi kwa watumiaji ambao hawataki kuyaona kwa kuwezesha udhibiti zaidi kwa watumiaji. Meta pia ina sera kadhaa mahususi kuhusu masuala ambayo pia inashughulikia kupitia sera ya picha za uchi (kama vile Sera ya Unyanyasaji wa Kingono wa Watu Wazima, na sera za Unyanyasaji wa Kingono wa Watoto, Dhuluma na Uchi) ambazo zinaweza kuimarishwa.
Bodi inabainisha kuwa mbinu za utekelezaji za Meta zinaripotiwa kusababisha idadi kubwa ya chanya za uwongo, au uondoaji kimakosa wa maudhui yasiyokiuka. Ripoti ya mwisho ya Meta ya Utekelezaji wa Viwango vya Jumuiya ya Instagram ( Aprili-Juni 2022) ilifichua kuwa, asilimia 21 ya uondoaji wa Picha za Uchi wa Watu Wazima na Shughuli za Ngono ambao ulikatiwa rufaa ulisababisha maudhui hayo kurejeshwa. Bodi pia ilipokea idadi kubwa ya maoni ya umma kuhusu maudhui kuondolewa kimakosa chini ya Sera ya Picha za Uchi za Watu Wazima.
Kutobaguliwa
Kuna ushahidi kwamba sera na utekelezaji wa Meta unaohusiana na Picha za Uchi za Watu Wazima na Shughuli za Ngono zinaweza kusababisha athari zisizo sawa kwa wanawake na watu wa LGBTQI+. Athari hizi zinaonekana katika sera na utekelezaji na hupunguza njia ambazo vikundi vinaweza kujieleza, kupinga ubaguzi na kuongeza mwonekano wao katika jamii.
Ingawa kesi hii iliwahusu watumiaji waliobadilisha jinsia na wasiokuwa na jinsia yoyote, hitilafu za utekelezaji katika kesi hii zinatokana na sera msingi ambayo pia inawaathiri wanawake, hasa kwa vile Meta inatumia mbinu ya 'chaguo-msingi kwa wanawake' katika maudhui ya picha za uchi. Kwa hivyo, sehemu hii inazingatia jinsi sera za Meta zinaathiri watu wa LGBTQI+ na wanawake. Idadi kubwa ya mawasilisho ya umma katika kesi hii yalitoa vielelezo vingi vya athari zinaweza kuwa katika sera hizi.
Haki ya uhuru wa kujieleza inahakikishwa kwa watu wote bila ubaguzi kuhusu “ngono” au “hadhi nyingine” (Kifungu cha 2, aya ya 1, ICCPR). Hii inajumuisha mwelekeo wa ngono na utambulisho wa kijinsia ( Toonen v. Australia (1994); A/HRC/19/41, aya ya 7). Sheria ya Kamati ya Haki za Kibinadamu inabainisha kwamba “sio kila utofautishaji unaotokana misingi iliyoorodheshwa katika kifungu cha 26 cha Mkataba unalingana na ubaguzi, mradi tu unatokana na vigezo vinavyofaa na vyenye lengo na kufuata lengo ambalo ni halali chini ya Mkataba” Nepomnyashchiy dhidi ya Urusi, Kamati ya Haki za Binadamu, 2018, aya ya 7.5 (CCPR/C/123/D/2318/2013).
Mkataba wa Kuondoa Aina Zote za Ubaguzi Dhidi ya Wanawake (CEDAW) inakataza “ubaguzi wowote, kutengwa au kizuizi chochote kinachofanywa kwa msingi wa jinsia ambacho kina athari au madhumuni ya kudhoofisha au kubatilisha utambuzi, starehe au mazoezi ya wanawake […] kwa msingi wa usawa wa wanaume na wanawake, haki za binadamu na uhuru msingi katika nyanja ya kisiasa, kiuchumi, kijamii, kitamaduni, kiraia au nyingine yoyote” (CEDAW, Art. 1). Bodi inabainisha kuwa mashirika ya kimataifa ya haki za binadamu hayajashughulikia athari za haki za binadamu za kuruhusu au kukataza picha za uchi za watu wazima zenye idhini na athari zake za kibaguzi.
Kanuni Elekezi za Umoja wa Mataifa zinasema kwamba “biashara zinapaswa kuwa waangalifu kabisa kwa athari zozote za haki za binadamu katika watu binafsi kutoka kwa vikundi au watu ambao wanaweza kuwa katika hatari kubwa ya kuathirika au kutengwa” ( UNGPs, Kanuni za 18 na 20). Mwandishi Maalum kuhusu uhuru wa kujieleza amezitaka kampuni za teknolojia “kutafuta na kuzingatia kikamilifu maswala ya jamii zilizo katika hatari ya kudhibitiwa na kubaguliwa kihistoria” ( A/HRC/38/35, aya ya 48). Kikundi Kazi cha Umoja wa Mataifa kuhusu Biashara na Haki za Binadamu pia kimependekeza kwamba makampuni ya teknolojia yahakikishe kwamba “uerevu buniwa na uwekaji kiotomatiki hauna athari zisizo na uwiano kwa haki za binadamu za wanawake” ( Kitabu cha Mwongozo wa Vipimo vya Jinsia).
Kwa kuzingatia umuhimu wa majukwaa ya mitandao ya kijamii kama uwanja wa watu binafsi wanaobaguliwa kujieleza, Bodi imeeleza mara kwa mara matarajio yake kwamba Meta iwe makini sana na uwezekano wa uondoaji wa maudhui kimakosa na, kuhusu au kuonyesha wanachama wa vikundi hivi. Kama Bodi ilivyobaini katika uamuzi wa "Mkanda wa Wampum" (2021-012-FB-UA) kuhusu usemi wa kisanii kutoka kwa watu wa Kiasili, haitoshi kutathmini utendakazi wa utekelezaji wa Meta wa sera ya Facebook ya Matamshi ya Chuki kwa idadi ya watumiaji kwa ujumla – athari kwa makundi maalum lazima izingatiwe. Vivyo hivyo, katika kesi ya “Kurejesha maneno ya Kiarabu”, Bodi ilithibitisha kwamba “udhibiti kupita kiasi wa matamshi ya watumiaji kutoka kwa vikundi vya watu wachache wanaonyanyaswa ni tishio kubwa kwa uhuru wao wa kujieleza” na ilionyesha wasiwasi wao kuhusu jinsi misamaha katika sera za Meta (katika kesi hiyo, sera ya Matamshi ya Chuki) ilitumika kwa makundi yaliyotengwa kujieleza ( 2022-003-IG-UA).
Matokeo ya uchaguzi wa Meta husababisha fursa tofauti za kujieleza zipatikane kwa wanawake, watu waliobadilisha jinsia, na watu wasiokuwa na jinsia yoyote kwenye majukwaa yake. Sera ya sasa ya Meta ya Picha za Uchi wa Watu Wazima na Shughuli za Ngono huchukulia matiti na chuchu za wanawake kama ngono asilia, na kwa hivyo zinaweza kupigwa marufuku, isipokuwa kama wamefanyiwa upasuaji au watafanyiwa upasuaji au wananyonyesha. Badala ya kuchukua hatua ili kuhakikisha kuwa udhibiti hauathiri kwa njia isiyo sawa baadhi ya vikundi, sera ya Meta inaimarisha na kuendeleza athari kama hizo kwa vikundi hivi.
Kesi hizi zinaangazia athari kubwa ya chaguo za sera za Meta kwa watu wanaojitambulisha kuwa LGBTQI+, kwani maudhui yalitambuliwa mara nyingi na viainishaji vya Picha za Uchi za Watu Wazima na Shughuli za Ngono licha ya kuwa nje ya upeo wa sera hiyo. Bodi inaamini kwamba kesi hizi ni ishara ya matatizo makubwa zaidi. Kwa mfano, Utafiti wa Haimson et al. uligundua kuwa watu waliobadilisha jinsia huripoti viwango vya juu vya maudhui kuondolewa na akaunti kufutwa, kwa kawaida kutokana na maudhui ya picha za uchi na ngono.
Utekelezaji wa uchaguo za sera za Meta pia una athari zisizo sawa kwa wanawake. Utafiti wa Witt, Suzor, na Higgins uligundua kuwa hadi asilimia 22 ya picha za miili ya wanawake ambazo ziliondolewa kwenye Instagram zilionekana kuwa chanya za uwongo. Athari tofauti katika miili ya wanawake pia ilibainishwa katika maoni ya umma (tazama, k.m, Maoni ya Umma 10616 ya Dkt. Zahra Stardust).
Msimamo huu chaguo-msingi wa uchi pia una athari kubwa katika miktadha ambapo wanawake wanaweza kijadi kwenda kifua wazi. Mwandishi Maalumu kuhusu uhamasishaji na ulinzi wa haki za uhuru wa maoni na kujieleza amezitaka kampuni zishirikiane na makundi ya kiasili duniani kote ili “kutengeneza viashirio bora vya kuzingatia muktadha wa kitamaduni na kisanii wakati wa kutathmini maudhui yanayoangazia picha za uchi” (aya ya 54, A/HRC/38/35).
Kando na masuala haya ya kutobaguliwa yanayohusiana na sera, kesi hizi pia ziliibua wasiwasi unaohusiana na utekelezaji wa kutokuwa na ubaguzi. Meta inapaswa kukumbuka kuwa maudhui kutoka kwa watumiaji wanaojitambulisha na makundi yaliyotengwa yamo katika hatari kubwa ya kuripotiwa mara kwa mara, ambapo watumiaji huripoti maudhui yasiyokiuka ili kuwaelemea au kuwanyanyasa watumiaji. Masuala haya pia yaliibuliwa na maoni kadhaa ya umma (tazama, k.m., Maoni ya Umma 10596 ya GLAAD na Maoni ya Umma 10628 ya The Human Rights Campaign Foundation).
Kesi hizi ziliangazia kwamba ripoti nyingi zinazotoa maoni mengi zinaweza kuongeza uwezekano wa uondoaji wa kimakosa. Hakika, katika kesi hii, ripoti nyingi za watumiaji zilisababisha ukaguzi wa binadamu ambao ulipata kuwa maudhui hayakiuki, lakini maudhui yaliendelea kuripotiwa hadi wakaguzi walipobaini kimakosa kuwa yanakiuka na wakayaondoa.
Meta inapaswa kutafuta kuunda na kutekeleza sera ambazo zinasaidia kurekebisha maswala haya yote. Hizi zinaweza kujumuisha sera zaidi zinazofanana zinazohusiana na picha za uchi zinazotumika bila ubaguzi kwa misingi ya jinsia au utambulisho wa kijinsia. Zinaweza pia kujumuisha uamuzi wenye muktadha zaidi wa maudhui ambayo ni ya ngono, mradi tu maamuzi kama hayo yanaepuka kutegemea vigezo vya ubaguzi katika kufanya maamuzi kama haya.
Bodi inabainisha kuwa Meta ina sera mahususi ya kushughulikia taswira ya mahaba bila ridhaa katika sera yake ya Unyanyasaji wa Kingono wa Watu Wazima. Huu umekuwa uwanja wa utekelezaji uliopewa kipaumbele na kampuni (angalia, kwa mfano, kuanzishwa kwao kwa teknolojia ya utambuzi wa kiotomatiki ili kukomesha picha zisizo za ridhaa kutumwa mara kwa mara). Wakati Meta inazingatia kubadilisha mbinu yake ya kudhibiti picha za uchi kwenye jukwaa, Meta inapaswa kuchunguza kwa karibu kiwango ambacho sera ya Picha za Uchi za Watu Wazima na Shughuli za Ngono hulinda dhidi ya kushiriki picha zisizo za ridhaa na kuelewa ikiwa mabadiliko katika sera ya Unyanyasaji wa Kingono wa Watu Wazima au utekelezaji wake unaweza kuhitajika ili kuimarisha ufanisi wake.
Bodi pia inatambua kuwa Meta inaweza kuwa na nia halali ya kuzuia maudhui ya ngono au ponografia kwenye jukwaa yake. Lakini Bodi inaamini kwamba malengo husika ya biashara yanaweza na yanapaswa kutimizwa kwa mbinu zinazowashughulikia watumiaji wote bila ubaguzi.
Baadhi ya wanachama wa Bodi wanaamini kuwa Meta inapaswa kujaribu kupunguza athari za ubaguzi katika sera zake za sasa kwa kupitisha sera ya picha za uchi za watu wazima ambayo haitegemei tofauti za jinsia. Walibainisha vifungu vya Mkataba wa Kutokomesha Aina Zote za Ubaguzi Dhidi ya Wanawake (CEDAW) kuhusu kuondoa dhana potofu za kijinsia (tazama, kwa mfano, Kifungu cha 5 na 10) na dhamira ya wazi ya Meta kwa CEDAW katika sera yake ya shirika la haki za binadamu. Walihitimisha kwamba, katika muktadha wa sera ya picha za uchi, viwango hivi vya kimataifa vya haki za binadamu na dhamira ya Meta yenyewe ya kutobagua, vinaunga mkono kuondoa tofauti potofu. Kundi hili la wanachama limehitimisha kuwa kugeukia sera isiyotegemea jinsia au tofauti za kijinsia itakuwa njia bora zaidi kwa Meta kutumia wajibu wake wa haki za binadamu kama biashara, kwa kuzingatia maadili na ahadi zake za shirika. Wanachama hawa wanaona kwamba kanuni na sera zinapaswa kubadilika ili kushughulikia mikataba ambayo ina athari za kibaguzi, kama vile aina nyingi za ubaguzi zilivyokuwa au zinaendelea kuenezwa na kuwa mkataba wa kijamii ulioenea.
Kulikuwa na kutoelewana kati ya Wanachama wa Bodi kuhusu masuala haya. Baadhi ya wanachama walikubali kimsingi kwamba Meta haipaswi kutegemea ngono au jinsia ili kupunguza kujieleza lakini walikuwa na shaka sana kuhusu uwezo wa Meta wa kushughulikia kwa ufanisi taswira ya mahaba bila ridhaa na madhara mengine yanayoweza kutokea bila sera ya uchi unaozingatia ngono na jinsia. Wanachama wengine wa Bodi wanaamini kwamba kwa sababu kanuni zinazotumika za haki za binadamu kuhusu kutobaguliwa huruhusu kutofautisha kwa misingi ya sifa zinazolindwa mradi tu “zinazingatia vigezo vinavyofaa na vyenye lengo na katika kutekeleza lengo ambalo ni halali chini ya Mkataba, ” ( Nepomnyashchiy dhidi ya Urusi, Kamati ya Haki za Binadamu, 2018, aya. 7.5 (CCPR/C/123/D/2318/2013), sera ya picha za uchi za ngono na mtu asiyependelea jinsia yoyote haihitajiki na inaweza kusababisha au kuzidisha madhara mengine.
Wanachama wa Bodi ambao wanaunga mkono sera ya picha za uchi za ngono ya watu wazima na watu wasiopendelea jinsia yoyote, wanatambua kuwa chini ya viwango vya kimataifa vya haki za binadamu vinavyotumika kwa majimbo, utofautishaji kwa misingi ya sifa zinazolindwa zinaweza kufanywa kwa kuzingatia vigezo vinavyofaa na vyenye lengo na zinapotimiza madhumuni halali. Hawaamini kuwa tofauti zilizo ndani ya sera ya Meta ya picha za uchi zinakidhi kiwango hicho. Wanabainisha zaidi kuwa, kama mfanyabiashara, Meta imetoa ahadi za haki za binadamu ambazo hazilingani na mbinu inayozuia kujieleza mtandaoni kulingana na mtazamo wa kampuni kuhusu ngono na jinsia.
Kiwango cha Jumuiya kuhusu Picha za Uchi za Watu Wazima na Shughuli za Ngono huathiri kwa njia isiyo sawa wanawake na watumiaji wa LGBTQI+ na hutegemea mitazamo ya dhamira na ya kukisia kuhusu jinsia ambayo haiwezi kutekelezeka wakati wa kujihusisha katika udhibiti wa maudhui kwa kiwango. Ikizingatiwa kwa kina, kwa kuzingatia mkanganyiko wa sheria na utekelezaji wake, na athari zisizo na uwiano na za kibaguzi za sera ya sasa ya Meta ya Picha za Uchi za Watu Wazima na Shughuli za Ngono, Bodi inapendekeza kwamba Meta ibainishe vigezo wazi, vinavyolengwa, vya kuheshimu haki ili kudhibiti kwa jumla sera yake ya Picha za Uchi za Watu Wazima, inayohakikisha utendaji wa watu wote ambao unaambatana na viwango vya kimataifa vya haki za binadamu, ikijumuisha bila ubaguzi kwa misingi ya jinsia au utambulisho wa kijinsia. Meta inapaswa kwanza kufanya tathmini ya kina ya athari za haki za binadamu ili kukagua athari za kupitishwa vigezo kama hivyo, ambavyo vinajumuisha ushirikishwaji wa washikadau kwa upana katika miktadha tofauti ya kiitikadi, kijiografia na kitamaduni. Kwa kiwango ambacho tathmini hii inapaswa kubainisha madhara yoyote yanayoweza kutokea, utekelezaji wa sera mpya unapaswa kujumuisha mpango wa kuyashughulikia. Bodi inaomba ripoti kuhusu tathmini na kupanga miezi sita kutoka tarehe ya kutolewa kwa uamuzi huu.
9. Uamuzi wa Bodi ya usimamizi
Bodi ya Usimamizi inabatilisha maamuzi ya kwanza ya Meta ya kuondoa machapisho yote mawili, na kuhitaji yarejeshwe.
10. Taarifa ya ushauri wa sera
Sera ya maudhui
1. Ili kuwatendea watumiaji wote kwa haki na kuwapa wasimamizi na umma viwango vinavyoweza kutekelezeka kuhusu picha za uchi, Meta inapaswa kufafanua vigezo vilivyo wazi, vyenye lengo, vinavyoheshimu haki ili kudhibiti sera yake ya Picha za Uchi wa Watu Wazima na Shughuli za Ngono, kuhakikisha kuwa watu wote wanatendewa sawa kwa kuzingatia viwango vya kimataifa vya haki za binadamu, na kujumuisha kutobaguliwa kwa misingi ya jinsia au utambulisho wa kijinsia. Meta inapaswa kwanza kufanya tathmini ya kina ya athari za haki za binadamu ili kukagua athari za kupitishwa vigezo kama hivyo, ambavyo vinajumuisha ushirikishwaji wa washikadau kwa upana katika miktadha tofauti ya kiitikadi, kijiografia na kitamaduni. Kwa kiwango ambacho tathmini hii inapaswa kubainisha madhara yoyote yanayoweza kutokea, utekelezaji wa sera mpya unapaswa kujumuisha mpango wa kuyashughulikia.
2. Ili kutoa uwazi kwa watumiaji zaidi, Meta inapaswa kuwapa watumiaji maelezo zaidi kuhusu “ofa au ombi” la ngono (ikiwemo viungo vya tovuti za wahusika wengine) na kinachojumuisha mikao ya kuchochea ngono katika Viwango vya Jamii vya umma. Bodi itazingatia pendekezo hili litakalotekelezwa wakati ufafanuzi wa masharti haya pamoja na mifano unapoongezwa kwenye Kiwango cha Jumuiya kuhusu Uombaji wa Ngono.
Utekelezaji
3. Ili kuhakikisha kuwa kigezo cha ndani cha Meta cha sera yake ya Uombaji wa Ngono hakisababishi uondoaji wa maudhui mengi kuliko jinsi sera inayotumika na umma inayvyoonyesha na ili maudhui yasiyo ya ngono yasiondolewe kimakosa, Meta inapaswa kurekebisha mwongozo wake wa mkaguzi wa ndani ili kuhakikisha kwamba vigezo vinaonyesha sheria zinazotumika na umma na vinahitaji muunganisho ulio wazi zaidi kati ya “ofa au ombi” na “kipengele cha kuchochea ngono.” Bodi itazingatia hili kutekelezwa wakati Meta itakapopatia Bodi miongozo yake ya ndani iliyosasishwa ambayo inaangazia vigezo hivi vilivyorekebishwa.
*Dokezo la kiutaratibu:
Maamuzi ya Bodi ya Usimamizi yanatayarishwa na majopo ya Wanachama watano na kuidhinishwa na wengi wa wanachama wa Bodi. Maamuzi ya Bodi hayawakilishi maoni ya kibinafsi ya Wanachama wote.
Kwa uamuzi wa kesi hii, utafiti huru ulipangwa kwa niaba ya Bodi. Taasisi huru ya utafiti yenye makao yake makuu katika Chuo Kikuu cha Gothenburg na iliyotoa timu ya zaidi ya wanasayansi wa kijamii 50 kutoka mabara sita, pamoja na zaidi ya wataalamu 3,200 wa kila nchi kutoka kote ulimwenguni, walitoa ushauri wa kitaalamu kuhusu muktadha wa jamii na kisiasa na utamaduni. Bodi pia ilisaidiwa na Duco Advisors, shirika la ushauri linalolenga miingiliano ya siasa za ulimwengu, uaminifu na usalama na teknolojia.
Volver a Decisiones de casos y opiniones consultivas sobre políticas