Decisão de múltiplos casos
Kauli Zinazolenga Watu wa Asili wa Australia
1 de Agosto de 2024
Mtumiaji alikata rufaa ya uamuzi wa Meta wa kuruhusu machapisho mawili ya Facebook, yote mawili yalishirikiwa na mtumiaji mwingine, ambayo yanajibu makala ya habari kwa maoni yanayolenga watu wa Asili ya Australia.
2 casos incluídos neste pacote
FB-CRZUPEP1
Kesi kuhusu matamshi ya chuki kwenye Facebook
FB-XJP78ARB
Kesi kuhusu matamshi ya chuki kwenye Facebook
Uamuzi wa ufupi huchunguza kesi ambapo Meta imebatilisha uamuzi wake wa kwanza kuhusu kipande cha maudhui baada ya Bodi kupeleka kesi hiyo kwa kampuni na kujumuisha taarifa kuhusu makosa ambayo Meta imekiri. Huwa unaidhinisha na jopo la Wanachama wa Bodi, badala ya Bodi kamili, hauhusishi maoni ya umma na hayana thamani ya kutumika katika marejeleo ya Bodi. Maamuzi kwa ufupi huleta mabadiliko moja kwa moja kwenye maamuzi ya Meta, yakitoa uwazi kuhusu masahihisho haya, huku pia yakitambua maeneo ambayo Meta inaweza kuboresha utekelezaji wake.
Muhtasari
Mtumiaji alikata rufaa ya uamuzi wa Meta wa kuruhusu machapisho mawili ya Facebook, yote mawili yalishirikiwa na mtumiaji mmoja, ambayo yanajibu makala ya habari kwa maoni yanayolenga watu wa Asili ya Australia. Baada ya Bodi kuifahamisha Meta kuhusu rufaa hizo, kampuni ilibatilisha maamuzi yake ya kwanza na kuondoa machapisho hayo mawili.
Kuhusu Kesi hizi
Kati ya Desemba 2023 na Januari 2024, mtumiaji wa Australia alishiriki machapisho mawili ya Facebook kuhusu watu wa Asili ya Australia. Chapisho la kwanza lina kiungo cha makala yanayotoa maelezo ya juhudi ya baraza la ardhi ya Asili ya kununua ardhi katika mbuga katika mojawapo ya viunga vya Sydney. Manukuu ya chapisho hilo yanawadai watu wa Asili “waondoke waende jangwani mahali ambapo wanastahili kuwa kwa kweli.” Chapisho la pili linashiriki makala kuhusu kukimbizwa kwa gari katika kaskazini mashariki ya Australia. Manukuu ya chapisho hilo linawadai “Wananchi wajinga wa asili ya Australia” kuwa katika kifungo gerezani pamoja na “kuchapwa viboko 100.”
Sera ya Meta ya Matamshi ya Chuki inapiga marufuku kauli zinazounga mkono au kutetea kutengwa au kutojumuishwa kwa watu kwa msingi wa kabila na mbari. Meta hasa inapiga marufuku maudhui yanayodai wazi “kufukuza vikundi fulani” na maudhui yanayounga mkono “kunyimana ufikiaji wa nafasi (halisi na za mtandaoni).” Sera hiyo pia inapiga marufuku “laana lengwa” na “ujumuishaji unaotaja udhalili,” ikiwa ni pamoja na “sifa za kiakili” zinazoelekezwa kwa mtu au kikundi cha watu kulingana na sifa zao zilizolindwa.
Baada ya Bodi kuwasilisha kesi hii kwa Meta, kampuni ilibaini kuwa vipande hivyo viwili vya maudhui vilikiuka sera yake dhidi ya Matamshi ya Chuki na uamuzi wa awali wa kuruhusu vipande hivyo viwili vya maudhui haukuwa sahihi. Kampuni hiyo kisha iliondoa maudhui hayo kwenye Facebook.
Meta ilielezea Bodi kwamba chapisho hilo linadai kutengwa kwa watu wa Asili ya Australia kutoka kwa ardhi ya mbuga na kwamba kauli “kuondolewa” kwa kuwarejelea ni mfano wa laana lengwa dhidi ya wanachama wa kikundi kinacholindwa. Isitoshe, Meta ilikiri kuwa istilahi “ratbag (mjinga)” ni ya matusi na ina maana inayojumuisha “mtu mjinga” katika Kiingereza cha Australia, kwa hivyo inakiuka sera ya Meta kuhusu Matamshi ya Chuki inayopiga marufuku kauli zinazorejelea wanachama wa kikundi cha sifa zilizolindwa kuwa ana akili duni.
Mamlaka na Upeo wa Bodi
Bodi ina mamlaka ya kukagua uamuzi wa Meta kufuatia rufaa kutoka kwa watumiaji ambao waliripoti maudhui ambayo yaliachwa (Kifungu cha 2 cha Mkataba, Sehemu ya 1; Sheria ndogo za Kifungu cha 3, Sehemu ya 1).
Meta inapokiri kwamba ilikosea na ibatilishe uamuzi wake katika kesi inayoshughulikiwa ili ikaguliwe na Bodi, Bodi inaweza kuchagua kesi hiyo ili kuifanyia uamuzi kwa ufupi (Sheria ndogo Kifungu cha 2, Sehemu ya 2.1.3). Bodi hukagua uamuzi wa kwanza ili kuongeza ufahamu wa michakato ya uratibu wa maudhui, kupunguza makosa na kuongeza haki kwa watumiaji wa Facebook, Instagram na Threads.
Umuhimu wa Kesi
Bodi imesisitiza mara kwa mara umuhimu maalum wa kutatua matamshi ya chuki yanayolenga vikundi ambavyo kihistoria vimekuwa vikibaguliwa na bado vinaendelea kubaguliwa dhidi ya ( Ubaguzi Afrika Kusini na Chapisho katika Kipolandi Ambalo Linalenga maamuzi ya Watu Waliobadilisha Jinsia). Pia Bodi imetoa wasiwasi mkali kwamba matendo ya Meta ya utekelezaji yanaweza kuathiri bila usawa watu wa Kwanza wa Taifa. Katika uamuzi wa Mshipi wa Wampum, Bodi ilitambua kwamba huku makosa hayawezi kuepukika, “aina za makosa na watu au jumuiya zinazobeba mzigo wa makosa hayo inaakisi uteuzi uliopangwa ambao lazima ufanyiwe tathmini na uchunguzi kila mara.” Katika kesi hiyo, Bodi ilisisitiza umuhimu wa Meta kufuatilia usahihi wa utekelezaji wake wa matamshi ya chuki si tu kwa ujumla bali kwa unyeti mahususi wa makosa ya utekelezaji ya "kategoria ndogo za maudhui ambapo maamuzi yasiyo sahihi yana athari inayoonekana wazi kwa haki za binadamu." Bodi ilielezea kuwa ilikuwa ni “wajibu wa Meta kuonyesha kwamba imefanya uchunguzi kuhusu haki za binadamu ili kuhakikisha kwamba mifumo yake inafanya kazi kwa usawa na haiendelezi ukandamizaji wa kihistoria na unaoendelea.
Kuhusu madai ya kutengwa, Bodi ilipendekeza kwamba Meta “inafaa kuandika upya thamani ya Meta ya ‘Usalama’ ili kuonyesha kwamba matamshi ya mtandaoni yanaweza kuhatarisha usalama wa kimwili wa watu na haki ya kuishi, pamoja na hatari za vitisho, kutengwa na kunyamazishwa,” (Tuhuma za Uhalifu katika Raya Kobo, pendekezo nambari 1). Utekelezaji wa pendekezo hili umeonyeshwa kupitia taarifa zilizochapishwa.
Uamuzi
Bodi imebatilisha maamuzi ya kwanza ya Meta ya kuruhusu maudhui hayo. Bodi inatambua masahihisho ambayo Meta ilifanya kwenye makosa yake ya kwanza baada ya Bodi kujulisha Meta kuhusu kesi hizo.
Voltar para Decisões de Casos e Pareceres Consultivos sobre Políticas